Posts

Showing posts from June, 2024

Dk. Mwinyi ahimiza matumizi nishati salama

Image
Apongeza ushirikiano wa Oryx, Vigor uwekezaji mradi wa gesi NA MWANDISHI MWAALUM RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amezipongeza kampuni za Oryx Gas Tanzania Ltd na kampuni ya TP Limited ambayo ni   kampuni tanzu ya Vigor Turky’s Group of Companies kwa kujenga bohari ya kwanza ya kuhifadhi nishati ya gesi ili kuongeza usambazaji wa gesi ya iliyokandamizwa visiwani humo. Akihutubia wananchi wa Zanzibar baada ya kuzindua bohari hiyo huko Mangapwani, mkoa wa Kaskazini Unguja Dk. Mwinyi alieleza hatua hiyo itachochea utekelezaji wa mkakati wa taifa wa ulinzi wa mazingira na ongezeko la matumizi ya nishati safi kwa shughuli mbali mbali. Alieleza uwepo wa bohari ya kuhifadhi gesi pamoja na miundombinu mingine ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa bandari jumuishi inayojengwa katika ukanda huo ambayo itahusika bandari ya meli za mafuta, gesi pamoja na shughuli nyingine. Alisema kuanzishwa kwa bohari ya kuhifadhi ya gesi Zanzibar kutaongeza chachu

‘Uchaguzi serikali za mitaa kuzingatia falsafa ya 4R’

Image
NA SAIDA ISSA, DODOMA IMEELEZWA kuwa uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024 utazingatia maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kama ambavyo amekuwa akizungumza katika majukwaa mbali mbali akisisitiza falsafa ya ‘4R’ kwa maana ya maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya. Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Festo Dugange, katika kikao cha viongozi wa dini, Asasi za Kiraia na Mashirika yasiyo ya Kiserikali kujadili rasimu ya kanuni za uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024. Ambapo alisema kuwa uchaguzi huo utazingatia maono hayo ya Mheshmiwa Rais ili kila chama kipate nafasi sawa katika uchaguzi. "Ndugu washiriki, rasimu za kanuni zilizoandaliwa ni kama ifuatavyo, Rasimu ya Kanuni za Uchaguzi wa Mwenyekiti wa Kijiji, Wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji na Mwenyekiti wa Kitongoji katika Mamlaka za Wilaya za Mwaka 2024”, alieleza. Aliongeza kuwa; “Rasim