Posts

Showing posts from September, 2021
Image
Sandra Nankomah, Lily Kadima kushiriki ‘Mashariki Music Festival’ NA MWANDISHI WETU WASANII Sandra Nankomah na Lily Kadima kutoka Uganda wametajwa kuwa ni miongoni mwa wasanii watakaoshiriki tamasha la muziki la ‘Mashariki Festival’, linalotarajiwa kufanyika Zanzibar baadae mwezi ujao. Akizungumza na waandishi wa habari, Mratibu wa tamasha hilo, John Kagaruki,alieleza kuwa tamasha hilo linafanyika kwa lengo la kupata fedha ziitakazosaidia maendeleo ya Chuo cha Muziki cha Nchi za Majahazi (DCMA). Mratibu wa tamasha 'Mashariki Music Festival' John Kagaruki (katikati) akiwa na Mtendaji Mkuu wa kampuni ya CPS Ltd, Tobias Dietzold (kushoto) na mtendaji wa chuo cha DCMA, Halda Alkanaan. Kagaruki alieleza kuwa, pamoja na wasanii hao, pia wasanii kutoka Kenya, Tanzania bara na Zanzibar wakiwemo wahitimu wa chuo hicho watafanya maonesho ya muziki na kazi nyengine za sanaa. Aliwataja wasanii na vikundi vitakavyotumbuiza kuwa ni Fadhilee Itulya na Makadem kutoka Kenya, Msafiri Zaw
Image
BASFU yafanya msako wanaokiuka sheria NA MWANDISHI WETU KATIKA kukabiliana na changamoto ya ukiukwaji wa maadili na sheria inayohusiana na upigaji wa muziki, Baraza la Sanaa, Sensa, Filamu na Utamaduni (BASFU), limefanya ukaguzi wa kushitukiza na kubaini uwepo wa kumbi za starehe na baa zinazopiga muziki bila kuwa na leseni ya kufanya hivyo. Ukaguzi huo uliofanyika usiku wa kuamkia Septemba 11, 2021 katika maeneo mbali mbali ya shehia za Nungwi, mkoa wa Kaskazini Unguja, ulibaini uwepo wa maeneo na waendesha shughuli za muziki wanaofanya shughuli hiyo kinyume na sheria. Akizungumza baada ya ukaguzi huo, mrajisi wabaraza hilo, Juma Chum Juma, alieleza kuwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria namba 7 ya mwaka 2013 inayotoa maelekezo namna ya kuendesha shughuli hizo. “Kwa mujibu wa sheria ya baraza, sehemu zote za burudani, biashara na maeneo ya umma yanakazwa kupiga muziki na shughuli nyengine za burudani bila ya kuwa na leseni,” alieleza Juma. Aliongeza kuwa hatua hiyo imelenga
Image
  Majaliwa aridhishwa hatua ya ujenzi reli ya SGR NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAM WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa Majaliwa (pichani kushoto), amekagua mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha Dar es Salaam hadi Kilosa, mkoani Morogoro na kueleza kuridhishwa na hatua ya ujenzi iliyofikiwa. Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana wakati akikagua maendeleo ya ujenzi ya mradi huo katika kituo cha Kwala kilichopo mkoani Pwani, ambacho kitatumika kama kituo kikuu cha kufanya matengenezo makubwa ya mabehewa na injini za treni. “Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amedhamiria kukamilisha ujenzi wa miradi yote iliyoanzishwa, hivyo Watanzania waendelee kuwa na imani na Serikali yao, na tunawahakikishia mradi huu utakamilika kwa wakati,”alisema Majaliwa Alieleza kuwa Maendeleo ya ujenzi huu yanatia matumaini na kazi inaendelea kwa ufanisi na eneo lililobaki la Pugu Dar es Salaam tunaamini litakamilika kwa wakati, nimeridhishwa na vituo vya abiria vilivyokamilika. Aidha, Waziri Mkuu
Image
Balozi Hamza ahimiza ushirikiano sensa ya majaribio NA MWANDISHI WETU KAMISAA wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 Zanzibar, Balozi Mohammed Haji Hamza, amewataka wananchi wa shehia ya Michungwani, wilaya ya Magharib ‘B’, kutoa ushirikiano kwa makarani wa sensa na kutoa taarifa sahihi katika sensa ya majaribio itakayofanyika baadae mwezi huu. Akizungumza katika   mkutano na   wananchi wa eneo la Misufini, katika shehia hiyo ikiwa ni muendelezo wa ziara zake za kukutana   na viongozi wa serikali, kijamii na wananchi kwa lengo la kutoa elimu na kuhamasisha jamii juu ya ushiriki wa   zoezi hilo. Alisema sensa ya watu na makaazi ndio njia pekee ya kupata taarifa za msingi zikiwemo za idadi ya watu na taarifa mbali mbali za upatikanaji wa huduma za jamii zitakazotumiwa na serikali na watunga sera kupanga mipango ya maendeleo ya nchi. “Kikawaida sensa hufanyika kila baada ya miaka 10 lakini kabla ya kuingia kwenye zoezi lenyewe hufanyika majaribio mwaka mmoja kabla ili kupima h
Image
Vyombo vya habari vyatakiwa kuzipa kipaumbele habari za viongozi wanawake NA MWINYIMVUA NZUKWI VYOMBO vya habari vimetakiwa kuongeza jitihada za kuwahamasisha wanawake kujiandaa kuwania nafasi za uongozi ili kutimiza azma ya serikali ya kuwa na uwakilishi sawa baina ya wanawake na wanaume kwenye vyombo vya maamuzi. Wito huo umetolewa na Mtafiti wa maswala ya habari na mawasiloiano, Dk. Aboubakar  Rajab (pichani), alipokuwa akiwasilisha matokeo ya utafiti kuhusu habari zinazowahusu wanawake viongozi, katika ofisi za Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA – Zanzibar), Tunguu, wilaya ya Kati Unguja. Alieleza kuwa katika kipindi cha mwezi novemba na disemba 2020, vyombo vya habari viliripoti kwa uchache habari za viongozi wanawake ikilinganishwa na viongozi wanaume jambo linanoibua hisia za upendeleo. Alisema ili kurekebisha hali hiyo, vyombo vya habari vinapaswa kuwa na mikakati madhubuti ya kuwajengea uwezo wanawake kuwa viongozi kwa kueleza mafanikio na changamoto zinaz