Absa Tanzania yahamasisha wajasiriamali kutumia huduma za kifedha
NA MWANDISHI WETU BENKI ya Absa Tanzania imeendelea kuhamasisha wanawake wajasiriamali kutumia huduma rasmi za kifedha ili kuimarisha biashara zao na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Hatua hiyo imeelezwa kuwa sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia huduma zinazolenga kuongeza ujuzi wa usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mitaji na matumizi ya teknolojia katika biashara. Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wajasiriamali Duniani jijini Dar es Salaam, ambayo Absa ilikuwa miongoni mwa wadau waliodhamini, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa benki hiyo, Victor Nchimbi, alisema benki hiyo inatambua mchango mkubwa wa wajasiriamali katika kukuza uchumi. MKUU wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Victor Nchimbi, akizungumza na wajasiriamali kuhusu huduma zinazotolewa na benki hiyo zinazowalenga wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wajasiriamali Duniani ambapo Absa ilikuwa moja ya taasisi zilizojitokeza kudh...