Posts

Hemed azindua programu ya malezi, makuzi ya awali ya mtoto

Image
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imezindua Programu Jumuishi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto pamoja na Kituo cha Kulelea Watoto katika Soko la Mwanakwerekwe, ikiwa ni hatua ya kuimarisha ustawi wa watoto na kuwawezesha wazazi kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji. Akizindua programu hiyo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi , Makamu wa Pili wa Rais, Hemed Suleiman Abdulla , alisema Serikali inaamini kuwa uwekezaji katika malezi na makuzi ya awali ya mtoto ni msingi wa kujenga taifa lenye afya, elimu bora na uchumi imara. Alisema programu hiyo itawaunganisha wazazi na walezi katika kupata huduma muhimu zinazohusu afya, lishe, ulinzi na maendeleo ya watoto tangu wakiwa wadogo. Hemed alisema Serikali imeendelea kuboresha mazingira ya malezi kwa kuanzisha vituo vya kulelea watoto katika masoko, hospitali na skuli za awali ili kuwawezesha wazazi kutekeleza majukumu yao bila kuwa na hofu kuhusu usalam...

Programu kuimarisha elimu Chaani yazinduliwa

Image
Waziri  Lela asema  itaongeza hamasa ya kujifunza  NA MWANDISHI WETU WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohamed Mussa, amesema programu ya kuimarisha elimu katika jimbo la Chaani itapunguza changamoto zinazowakabili wazazi na walezi katika kugharamia mahitaji ya wanafunzi, hususani gharama za kambi za masomo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu hiyo uliofanyika katika viwanja vya Skuli ya Chaani Masingini, alisema Serikali ya awamu ya nane inaendelea kuitanguliza sekta ya elimu kwa kuimarisha miundombinu, kuongeza vifaa vya kufundishia na kujifunzia pamoja na kuboresha mazingira ya kujifunzia katika ngazi zote. WAZIRI Lela,  Mbunge na Mwakilishi wa jimbo la Chaani wakikabidhi moja ya makoksi ya karatasi kwa mmoja ya walimu wakuu skuli za jimbo kwa ajili ya mitihani ya kujiandaa na mitihani ya taifa  ya wanafunzi wa skuli zao. Alisema dhamira hiyo inaonekana kupitia ongezeko la bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, ambapo kwa ...

Uwazi matumizi ya bahari nyenzo muhimu kulinda uchumi wa Afrika – Tony Long

Image
NA MWANDISHI WETU MKURUGENZI Mtendaji wa Global Fishing Watch, Tony Long (pichani) amesema uwazi katika shughuli za baharini ni msingi muhimu wa kulinda rasilimali za bahari, kuimarisha uchumi wa Afrika na kuhakikisha usalama wa chakula kwa mamilioni ya wananchi wanaotegemea sekta ya uvuvi. Long alisema kwa karne nyingi jamii za pwani ya mashariki mwa Afrika zimeitumia Bahari ya Hindi kama chanzo cha biashara, ajira na maendeleo, huku akieleza kuwa umuhimu wa bahari unaendelea kuongezeka wakati ambapo uchumi wa buluu unatajwa kuwa miongoni mwa nguzo kuu za maendeleo ya bara. Alisema sekta za uvuvi na ufugaji wa samaki huchangia takribani dola bilioni 24 za Marekani kila mwaka katika uchumi wa Afrika, wakati thamani ya uchumi wa buluu wa bara hilo ikikadiriwa kufikia dola bilioni 300. Hata hivyo, Long alisema ukuaji huo unakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na kukosekana kwa uwazi katika shughuli nyingi za uvuvi wa baharini. Akinukuu matokeo ya utafiti wa mwaka 2024 uliofanywa na Gl...

Absa Tanzania yahamasisha wajasiriamali kutumia huduma za kifedha

Image
NA MWANDISHI WETU BENKI ya Absa Tanzania imeendelea kuhamasisha wanawake wajasiriamali kutumia huduma rasmi za kifedha ili kuimarisha biashara zao na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Hatua hiyo imeelezwa kuwa sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia huduma zinazolenga kuongeza ujuzi wa usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mitaji na matumizi ya teknolojia katika biashara. Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wajasiriamali Duniani jijini Dar es Salaam, ambayo Absa ilikuwa miongoni mwa wadau waliodhamini, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa benki hiyo, Victor Nchimbi, alisema benki hiyo inatambua mchango mkubwa wa wajasiriamali katika kukuza uchumi. MKUU wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Victor Nchimbi, akizungumza na wajasiriamali kuhusu huduma zinazotolewa na benki hiyo zinazowalenga wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wajasiriamali Duniani ambapo Absa ilikuwa moja ya taasisi zilizojitokeza kudh...

Wafikieni watumishi wa ngazi za juu, viongozi waandamizi – Mhandisi Zena

Image
NA MWANAJUMA SAID, IPA KATIBU wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Zena Ahmed Said, amelitaka Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar (IPA) kuwafikia watumishi wa kada za juu na viongozi waandamizi ili kuongeza ufanisi katika usimamizi na utoaji wa huduma za umma. Akizungumza wakati wa mahafali ya 18 ya chuo hicho huko Tunguu, alisema kuwa kwa muda mrefu IPA inatoa mafunzo ya muda mfupi yanayolenga zaidi watumishi wa kada za chini na kati, wakati kundi la viongozi wa ngazi za juu likibaki nyuma kupata mafunzo maalum yanayohitajika katika nafasi zao pekee. “Kuna haja sasa kuelekeza nguvu za kuwafikia watumishi wa kada za juu na viongozi. Ni muhimu viongozi wa ngazi zote wafikiwe kulingana na mahitaji yao ya mafunzo na upatikanaji wao”, alisema Mhandisi Zena. Alisema kuimarika kwa mafunzo hayo kutachochea maboresho ya mifumo ya uongozi, kuongeza uwajibikaji na kuleta matokeo chanya kwa wananchi katika taasisi za umma. KATIBU wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiong...

POSTA TANZANIA YATUNUKIWA CHETI CHA USALAMA NA UPU

Image
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM  SHIRIKA la Posta Tanzania limetunukiwa Cheti cha Usalama cha Kimataifa (S58 & S59) kutoka Umoja wa Posta Duniani (UPU), kufuatia mafanikio katika zoezi la tathmini ya usalama wa mifumo, miundombinu na taratibu za utoaji huduma lililokamilika Novemba 7, 2025.   Cheti hicho cha Daraja ‘A’ (tuzo ya dhahabu) kimetolewa rasmi, Novemba 24, 2025 na Mkurugenzi Mkuu wa UPU, Masahiko Metoki, mara baada ya timu ya wataalamu wa kufanya ukaguzi wa kina kwa muda wa wiki moja uliolenga kuhakiki viwango vya usalama wa Shirika katika kulinda mizigo, barua na taarifa nyeti zinazopitia mnyororo wa huduma za posta. Katika zoezi hilo, Shirika la Posta Tanzania limepata alama 598 kati ya 640, likitimiza kwa ufanisi vigezo vyote vya kupewa cheti hicho cha heshima kinachotolewa kwa taasisi za posta zinazofikia viwango vya juu vya usalama wa kimataifa. Wakipokea cheti hicho, Caroline Kanuti kwa niaba ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, pamoja...

Vyombo vya habari vinapaswa kusimamia mshikamano wa Afrika - UAJ

Image
NA MWANDISHI MAALUM, CAIRO MSHAURI wa Baraza Kuu la Usimamizi wa Vyombo vya Habari nchini Misri, Reem Hindi, ameeleza haja ya vyombo vya habari barani Afrika kusimamia msingi wa mshikamano wa Kiafrika ili kustawisha maendeleo ya bara na tasnia ya habari kwa ujumla. Alitoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya 61 yaliyoandaliwa na Umoja wa Waandishi wa Habari wa Afrika (UAJ) kwa kushirikiana na Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari yanayoendelea jijini Cairo, Misri yanayoshirikisha waandishi wa habari kutoka mataifa 20 ya Afrika huku Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) ukiwakilishwa na mwanachama wa Klabu ya Waaandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Khairat Haji Ali. Mshauri huyo aliweka wazi dhamira ya nchi hiyo kuunga mkono jitihada za UAJ za kujenga weledi na uhuru wa vyombo vya habari barani Afrika kama miongoni mwa mikakati ya kukuza kasi ya maendeleo na demokrasia. “Kupitia mafunzo, mijadala na kubadilishana uzoefu, vyombo vya habari vitaweza kusaidia nchi za ...