Posts

Absa Tanzania yahamasisha wajasiriamali kutumia huduma za kifedha

Image
NA MWANDISHI WETU BENKI ya Absa Tanzania imeendelea kuhamasisha wanawake wajasiriamali kutumia huduma rasmi za kifedha ili kuimarisha biashara zao na kuchangia ukuaji wa uchumi wa taifa. Hatua hiyo imeelezwa kuwa sehemu ya jitihada za benki hiyo katika kuwawezesha wanawake kiuchumi kupitia huduma zinazolenga kuongeza ujuzi wa usimamizi wa fedha, upatikanaji wa mitaji na matumizi ya teknolojia katika biashara. Akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wajasiriamali Duniani jijini Dar es Salaam, ambayo Absa ilikuwa miongoni mwa wadau waliodhamini, Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa benki hiyo, Victor Nchimbi, alisema benki hiyo inatambua mchango mkubwa wa wajasiriamali katika kukuza uchumi. MKUU wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Absa Tanzania, Victor Nchimbi, akizungumza na wajasiriamali kuhusu huduma zinazotolewa na benki hiyo zinazowalenga wafanyabiashara wadogo na wa kati, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wajasiriamali Duniani ambapo Absa ilikuwa moja ya taasisi zilizojitokeza kudh...

Wafikieni watumishi wa ngazi za juu, viongozi waandamizi – Mhandisi Zena

Image
NA MWANAJUMA SAID, IPA KATIBU wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Zena Ahmed Said, amelitaka Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar (IPA) kuwafikia watumishi wa kada za juu na viongozi waandamizi ili kuongeza ufanisi katika usimamizi na utoaji wa huduma za umma. Akizungumza wakati wa mahafali ya 18 ya chuo hicho huko Tunguu, alisema kuwa kwa muda mrefu IPA inatoa mafunzo ya muda mfupi yanayolenga zaidi watumishi wa kada za chini na kati, wakati kundi la viongozi wa ngazi za juu likibaki nyuma kupata mafunzo maalum yanayohitajika katika nafasi zao pekee. “Kuna haja sasa kuelekeza nguvu za kuwafikia watumishi wa kada za juu na viongozi. Ni muhimu viongozi wa ngazi zote wafikiwe kulingana na mahitaji yao ya mafunzo na upatikanaji wao”, alisema Mhandisi Zena. Alisema kuimarika kwa mafunzo hayo kutachochea maboresho ya mifumo ya uongozi, kuongeza uwajibikaji na kuleta matokeo chanya kwa wananchi katika taasisi za umma. KATIBU wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiong...

POSTA TANZANIA YATUNUKIWA CHETI CHA USALAMA NA UPU

Image
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM  SHIRIKA la Posta Tanzania limetunukiwa Cheti cha Usalama cha Kimataifa (S58 & S59) kutoka Umoja wa Posta Duniani (UPU), kufuatia mafanikio katika zoezi la tathmini ya usalama wa mifumo, miundombinu na taratibu za utoaji huduma lililokamilika Novemba 7, 2025.   Cheti hicho cha Daraja ‘A’ (tuzo ya dhahabu) kimetolewa rasmi, Novemba 24, 2025 na Mkurugenzi Mkuu wa UPU, Masahiko Metoki, mara baada ya timu ya wataalamu wa kufanya ukaguzi wa kina kwa muda wa wiki moja uliolenga kuhakiki viwango vya usalama wa Shirika katika kulinda mizigo, barua na taarifa nyeti zinazopitia mnyororo wa huduma za posta. Katika zoezi hilo, Shirika la Posta Tanzania limepata alama 598 kati ya 640, likitimiza kwa ufanisi vigezo vyote vya kupewa cheti hicho cha heshima kinachotolewa kwa taasisi za posta zinazofikia viwango vya juu vya usalama wa kimataifa. Wakipokea cheti hicho, Caroline Kanuti kwa niaba ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, pamoja...

Vyombo vya habari vinapaswa kusimamia mshikamano wa Afrika - UAJ

Image
NA MWANDISHI MAALUM, CAIRO MSHAURI wa Baraza Kuu la Usimamizi wa Vyombo vya Habari nchini Misri, Reem Hindi, ameeleza haja ya vyombo vya habari barani Afrika kusimamia msingi wa mshikamano wa Kiafrika ili kustawisha maendeleo ya bara na tasnia ya habari kwa ujumla. Alitoa rai hiyo wakati akifungua mafunzo ya 61 yaliyoandaliwa na Umoja wa Waandishi wa Habari wa Afrika (UAJ) kwa kushirikiana na Baraza Kuu la Udhibiti wa Vyombo vya Habari yanayoendelea jijini Cairo, Misri yanayoshirikisha waandishi wa habari kutoka mataifa 20 ya Afrika huku Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) ukiwakilishwa na mwanachama wa Klabu ya Waaandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), Khairat Haji Ali. Mshauri huyo aliweka wazi dhamira ya nchi hiyo kuunga mkono jitihada za UAJ za kujenga weledi na uhuru wa vyombo vya habari barani Afrika kama miongoni mwa mikakati ya kukuza kasi ya maendeleo na demokrasia. “Kupitia mafunzo, mijadala na kubadilishana uzoefu, vyombo vya habari vitaweza kusaidia nchi za ...

'Zanzibar Matibabu Card' yashinda tuzo ya WSIS

Image
NA MWANDISHI MAALUM, USWISI WIZARA ya Afya Zanzibar imetunukiwa tuzo ya kimataifa ya ‘ World Summit on the Information Society’ (WSIS) kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mfumo wa matibabu kwa njia ya kadi maalum ya kidijitali ijulikanayo kama ‘ Zanzibar Matibabu Card’ , ambao umewezesha utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi kupitia teknolojia. Hafla ya kukabidhi tuzo hiyo ilifanyika Geneva, Uswisi na kuhudhuriwa na Waziri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania, Jerry Slaa, Balozi wa Tanzania Geneva, Abdallah Possi, pamoja na wajumbe kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar (e-GAZ) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Waziri wa Afya Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui,   alisema mpango huo ni uthibitisho wa dhamira ya taifa kutumia teknolojia kuboresha maisha ya wananchi. Alieleza kuwa mfumo huo umeunganisha vituo vyote vya afya vya umma na taarifa za m...

Ufaulu kidato cha sita watahiniwa wa skuli juu

Image
NECTA yazuia matokeo ya watahiniwa 244 NA MWANDISHI WETU KATIBU Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Prof. Said Mohammed (pichani), amesema ufaulu wa watahiniwa wa skuli kwa mwaka 2025 umeongezeka kwa asilimia 0.03 huku ufaulu wa watahiniwa wa kujitegemea ukishuka kwa asilimia 2.64 ukilinganishwa na mwaka jana. Aliyasema hayo wakati akitangaza matokeo ya mitihani ya kidatu cha sita (ACSEE), ualimu daraja la tatu A (GATCE), mtihani wa ualimu daraja la A kozi maalumu (GATSCCE), mtihani wa stashahada ya ualimu wa sekondari (DSEE) iliyofanyika mwezi Mei 2025. Alieleza kuwa hali ya ufaulu wa kijinsia ni sawa kati ya wanawake na wanaume kwa asilimia 93.34 na kubainisha kuwa walioshindwa kufanya mitihani kwa watahiniwa wa skuli ni 68 sawa na asilimia 0.05. Aidha alifafanua kuwa watahiniwa wa skuli waliofaulu ni 125,779 sawa na asilimia 99.95 ya watahiniwa waliofanya mitihani, ukilinganisha na watahiniwa 103,252 sawa na asilimia 99.92 ya watahiniwa wa skuli kwa mwaka jana. “Mwak...

NBC yaahidi makubwa ligi kuu Tanzania bara

Image
NA MWANDISHI WETU MDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) jana ilikabidhi kombe la ubingwa wa Ligi Kuu ya soka ya NBC (NBCPL) kwa timu ya Yanga SC ya jijini Dar es Salaam iliyoibuka bingwa wa kombe hilo msimu wa mwaka 2024/2025. MAKAMU wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi (kushoto) wakikabidhi kikombe cha ubingwa wa Ligi KuuTanzania Bara (NBCPL) kwa nahodha Yanga SC, Bakari Mwamnyeto. Hafla ya kukabidhi ubingwa huo ilifanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa, jijini Dare es Salaam baada ya mchezo wa mwisho wa ligi hiyo baina ya mabingwa hao na Simba SC ya jijini uliomalizika kwa yanga kuibuka na ushindi wa magoli 2 - 0. Hafla hiyo iliongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Athuman Nyamlani na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, ambao kwa pamoja walikabidhi kombe hilo. Akizungumza baada ya tukio hilo, Sabi pamoja na kuwapon...