Programu kuimarisha elimu Chaani yazinduliwa
Waziri Lela asema itaongeza hamasa ya kujifunza NA MWANDISHI WETU WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohamed Mussa, amesema programu ya kuimarisha elimu katika jimbo la Chaani itapunguza changamoto zinazowakabili wazazi na walezi katika kugharamia mahitaji ya wanafunzi, hususani gharama za kambi za masomo. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu hiyo uliofanyika katika viwanja vya Skuli ya Chaani Masingini, alisema Serikali ya awamu ya nane inaendelea kuitanguliza sekta ya elimu kwa kuimarisha miundombinu, kuongeza vifaa vya kufundishia na kujifunzia pamoja na kuboresha mazingira ya kujifunzia katika ngazi zote. WAZIRI Lela, Mbunge na Mwakilishi wa jimbo la Chaani wakikabidhi moja ya makoksi ya karatasi kwa mmoja ya walimu wakuu skuli za jimbo kwa ajili ya mitihani ya kujiandaa na mitihani ya taifa ya wanafunzi wa skuli zao. Alisema dhamira hiyo inaonekana kupitia ongezeko la bajeti ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, ambapo kwa ...