Uwazi matumizi ya bahari nyenzo muhimu kulinda uchumi wa Afrika – Tony Long
NA MWANDISHI WETU MKURUGENZI Mtendaji wa Global Fishing Watch, Tony Long (pichani) amesema uwazi katika shughuli za baharini ni msingi muhimu wa kulinda rasilimali za bahari, kuimarisha uchumi wa Afrika na kuhakikisha usalama wa chakula kwa mamilioni ya wananchi wanaotegemea sekta ya uvuvi. Long alisema kwa karne nyingi jamii za pwani ya mashariki mwa Afrika zimeitumia Bahari ya Hindi kama chanzo cha biashara, ajira na maendeleo, huku akieleza kuwa umuhimu wa bahari unaendelea kuongezeka wakati ambapo uchumi wa buluu unatajwa kuwa miongoni mwa nguzo kuu za maendeleo ya bara. Alisema sekta za uvuvi na ufugaji wa samaki huchangia takribani dola bilioni 24 za Marekani kila mwaka katika uchumi wa Afrika, wakati thamani ya uchumi wa buluu wa bara hilo ikikadiriwa kufikia dola bilioni 300. Hata hivyo, Long alisema ukuaji huo unakabiliwa na changamoto kubwa kutokana na kukosekana kwa uwazi katika shughuli nyingi za uvuvi wa baharini. Akinukuu matokeo ya utafiti wa mwaka 2024 uliofanywa na Gl...