Posts

Showing posts from July, 2024

Treni ya SGR ina faida kiuchumi, kijamii - RC Senyamule

Image
NA SAIDA ISSA, DODOMA MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule (pichani), amesema usafiri wa treni ya kisasa una faida nyingi za kiuchumi na kijamii kwani utapunguza muda wa safari kutoka saa nane hadi tisa kwa usafiri wa mabasi hadi saa tatu na nusu kwa safari ya Dodoma – Dar es salam. Hayo ameyaeleza Jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa rasmi wa safari za treni ya kisasa kwenda Morogoro – Dar es salaam kutokea Dodoma utakaofanyika Agosti 1, 2024 katika stendi kuu reli jijini Dodoma. Senyamule amesema kuwa treni hiyo ya umeme itawawezesha wafanyabiashara kusafiri kutoka mkoa mmoja wa Dar es Salaam au Dodoma na kurudi kuendelea na biashara zao ndani ya muda mfupi. "Kituo hiki cha treni kina sehemu mbali mbali ikiwemo sehemu zakufanyia biashara makundi, waje wafanyabiashara wanaotaka kufanyia biashara zao hapa, majengo ni ya kisasa, waje wawekeze kwani mkoa wa Dodoma ni mkoa wenye utalii, wageni watakao kuja na treni watajifunza na k

Mifumo ulinzi mali za serikali kuimarisha uchumi

Image
NA MWANDISHI WETU NAIBU Katibu Mkuu Mawasiliano wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Dk. Mzee Suleiman Mndewa, amesema hatua ya kuimarisha uchumi wa kidigitali, itafikiwa endapo watumishi wa umma watatumia mifumo itakayosaidia mali za serikali kubaki salama. Naibu huyo, amesema hayo Julai 15, 2024 alipofungua mafunzo kwa watendaji wa taasisi sehemu ya IT, wahasibu, wakaguzi wa ndani na wasimamizi wa mali za serikali, juu ya matumizi ya mifumo katika kurikodi mali za serikali yaliofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Uwanja wa ndege Zanzibar. NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Dk. Mzee Suleiman Mdewa, akifungua mafunzo ya usimamizi wa mali za umma kwa njia ya kidigitali yaliowashirikisha maofisa TEHAMA na wasimamizi wa mali za umma wa Serikali. Amesema mfumo wa udhibiti wa mali za serikali ni muhimu katika uchumi wa kidigitali, kwani utakapotumika vizuri utairahisisha kufanyika maamuzi kwa urahisi huku ikiwa na vielelezo vya ushahidi wa uhak