Posts

Showing posts from September, 2024

Jaji Mstaafu Luanda amrithi Jaji Mlay MCT

Image
NA MWANDISHI MAALUM MKUTANO Mkuu wa 26 wa wanachama wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), umemchagua Jaji Mstaafu Bernad Luanda (pichani) kuwa R ais wa baraza hilo kuziba nafasi iliyoachwa na jaji mstaafu Juxon Mlay,  aliyefariki dunia mapema mwaka huu. Akizungumza baada ya uchaguzi huo, Katibu Mtendaji wa baraza hilo, Ernest Sungura, amewashukuru wanachama walioshiriki mkutano huo na kueleza kuwa baraza limejipanga kuimarisha huduma zake kwa wananchama ikiwemo kuwanoa waandishi wa habari. Amesema, kuanzia mwaka ujao MCT itakua inatekeleza mradi mkubwa utakaojulikana kwa jina la ‘WAJIBIKA’ ambao utakuwa wa miaka saba ambapo utakuwa na thamani ya  pauni milioni 30, utakaogusa kila eneo, ikiwemo kuwajengea uwezo hata waandishi wa habari mmoja mmoja, kupiti vyombo vyao. Alieleza kuwa, jingine ambalo litafanyika mwakani, ni sherehe kubwa na za aina yake, ya mafanikio ya ‘MCT’ kwa miaka 30, tokea lilipoanzishwa mwaka 1995. Katibu Mtendaji huyo, aliwataka wanachama wenye madeni, ambay...

UVCCM yalaani wanaochochea uvunjifu wa amani

Image
NA SAIDA ISSA, DODOMA BARAZA Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) taifa limelaani vikali tabia ya baadhi ya watu, taasisi na jumuiya za kimataifa zenye tabia ya kutumia vijana kuharibu na kubeza amani, umoja na mshikamano wa taifa. Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dk. Emenuel Nchimbi (kushoto) akizungumza wakati kikao cha Baraza Kuu la UVCCM. Kulia ni Mwenyekiti Taifa wa UVCCM. Kauli hiyo ilitolewa jijini Dodoma na Mwenyekiti wa umoja huo Mohamed Ali Mohamed ‘Kawaida’ alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kikao cha kawaida cha baraza kuu la umoja huo lililokutana hivi karibuni. "UVCCM tunalaani vikali vitengo viovu vinavyowatumia vijana ama kuwahusisha katika matukio hayo na hatutafumbia macho matukio hayo", alisema Mwenyekiti huyo. Aidha aliongeza kuwa Baraza hilo linawataka vijana wote wenye sifa kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kujiandikisha katika daftari la mkazi,kugombea na kupiga kura na kwamb...