UVCCM yalaani wanaochochea uvunjifu wa amani

NA SAIDA ISSA, DODOMA

BARAZA Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) taifa limelaani vikali tabia ya baadhi ya watu, taasisi na jumuiya za kimataifa zenye tabia ya kutumia vijana kuharibu na kubeza amani, umoja na mshikamano wa taifa.


Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dk. Emenuel Nchimbi (kushoto) akizungumza wakati kikao cha Baraza Kuu la UVCCM. Kulia ni Mwenyekiti Taifa wa UVCCM.

Kauli hiyo ilitolewa jijini Dodoma na Mwenyekiti wa umoja huo Mohamed Ali Mohamed ‘Kawaida’ alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kikao cha kawaida cha baraza kuu la umoja huo lililokutana hivi karibuni.

"UVCCM tunalaani vikali vitengo viovu vinavyowatumia vijana ama kuwahusisha katika matukio hayo na hatutafumbia macho matukio hayo", alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha aliongeza kuwa Baraza hilo linawataka vijana wote wenye sifa kujitokeza kwa wingi kwenye zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa kwa kujiandikisha katika daftari la mkazi,kugombea na kupiga kura na kwamba UVCCM itawaunga mkono.

"Baraza kuu la umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi kwa kauli moja tunazipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar chini ya Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa namna zinavyoendelea kuwatumikia wananchi kwa vitendo kupitia utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi yam waka 2020 - 2025", alisema.

  Mwenyekiti Taifa wa UVCCM Taifa, Mohamed Ali Mohamed 'Kawaida' (katikati) akiongoza kikao cha Baraza Kuu la UVCCM Taifa kilichohudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dk. Emanuel Nchimbi (wa pili kushoto) na Naibu Katibu Mkuu wa CCM bara, John Mongela (wa kwanza kulia) .

Comments

Popular posts from this blog

ZAMECO yakerwa na video ya udhalilishaji mtandaoni

Airtel Foundation yazindua mpango wa udhamini wa masomo kwa vijana

SMZ yawaita vijana kushiriki kilimo