Posts

Showing posts from July, 2025

'Zanzibar Matibabu Card' yashinda tuzo ya WSIS

Image
NA MWANDISHI MAALUM, USWISI WIZARA ya Afya Zanzibar imetunukiwa tuzo ya kimataifa ya ‘ World Summit on the Information Society’ (WSIS) kutokana na mafanikio ya utekelezaji wa mfumo wa matibabu kwa njia ya kadi maalum ya kidijitali ijulikanayo kama ‘ Zanzibar Matibabu Card’ , ambao umewezesha utoaji wa huduma bora za afya kwa wananchi kupitia teknolojia. Hafla ya kukabidhi tuzo hiyo ilifanyika Geneva, Uswisi na kuhudhuriwa na Waziri wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa tanzania, Jerry Slaa, Balozi wa Tanzania Geneva, Abdallah Possi, pamoja na wajumbe kutoka Mamlaka ya Serikali Mtandao Zanzibar (e-GAZ) na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Akipokea tuzo hiyo kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Waziri wa Afya Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui,   alisema mpango huo ni uthibitisho wa dhamira ya taifa kutumia teknolojia kuboresha maisha ya wananchi. Alieleza kuwa mfumo huo umeunganisha vituo vyote vya afya vya umma na taarifa za m...

Ufaulu kidato cha sita watahiniwa wa skuli juu

Image
NECTA yazuia matokeo ya watahiniwa 244 NA MWANDISHI WETU KATIBU Mtendaji Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Prof. Said Mohammed (pichani), amesema ufaulu wa watahiniwa wa skuli kwa mwaka 2025 umeongezeka kwa asilimia 0.03 huku ufaulu wa watahiniwa wa kujitegemea ukishuka kwa asilimia 2.64 ukilinganishwa na mwaka jana. Aliyasema hayo wakati akitangaza matokeo ya mitihani ya kidatu cha sita (ACSEE), ualimu daraja la tatu A (GATCE), mtihani wa ualimu daraja la A kozi maalumu (GATSCCE), mtihani wa stashahada ya ualimu wa sekondari (DSEE) iliyofanyika mwezi Mei 2025. Alieleza kuwa hali ya ufaulu wa kijinsia ni sawa kati ya wanawake na wanaume kwa asilimia 93.34 na kubainisha kuwa walioshindwa kufanya mitihani kwa watahiniwa wa skuli ni 68 sawa na asilimia 0.05. Aidha alifafanua kuwa watahiniwa wa skuli waliofaulu ni 125,779 sawa na asilimia 99.95 ya watahiniwa waliofanya mitihani, ukilinganisha na watahiniwa 103,252 sawa na asilimia 99.92 ya watahiniwa wa skuli kwa mwaka jana. “Mwak...