Posts

Showing posts from November, 2025

Wafikieni watumishi wa ngazi za juu, viongozi waandamizi – Mhandisi Zena

Image
NA MWANAJUMA SAID, IPA KATIBU wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Zena Ahmed Said, amelitaka Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar (IPA) kuwafikia watumishi wa kada za juu na viongozi waandamizi ili kuongeza ufanisi katika usimamizi na utoaji wa huduma za umma. Akizungumza wakati wa mahafali ya 18 ya chuo hicho huko Tunguu, alisema kuwa kwa muda mrefu IPA inatoa mafunzo ya muda mfupi yanayolenga zaidi watumishi wa kada za chini na kati, wakati kundi la viongozi wa ngazi za juu likibaki nyuma kupata mafunzo maalum yanayohitajika katika nafasi zao pekee. “Kuna haja sasa kuelekeza nguvu za kuwafikia watumishi wa kada za juu na viongozi. Ni muhimu viongozi wa ngazi zote wafikiwe kulingana na mahitaji yao ya mafunzo na upatikanaji wao”, alisema Mhandisi Zena. Alisema kuimarika kwa mafunzo hayo kutachochea maboresho ya mifumo ya uongozi, kuongeza uwajibikaji na kuleta matokeo chanya kwa wananchi katika taasisi za umma. KATIBU wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiong...

POSTA TANZANIA YATUNUKIWA CHETI CHA USALAMA NA UPU

Image
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM  SHIRIKA la Posta Tanzania limetunukiwa Cheti cha Usalama cha Kimataifa (S58 & S59) kutoka Umoja wa Posta Duniani (UPU), kufuatia mafanikio katika zoezi la tathmini ya usalama wa mifumo, miundombinu na taratibu za utoaji huduma lililokamilika Novemba 7, 2025.   Cheti hicho cha Daraja ‘A’ (tuzo ya dhahabu) kimetolewa rasmi, Novemba 24, 2025 na Mkurugenzi Mkuu wa UPU, Masahiko Metoki, mara baada ya timu ya wataalamu wa kufanya ukaguzi wa kina kwa muda wa wiki moja uliolenga kuhakiki viwango vya usalama wa Shirika katika kulinda mizigo, barua na taarifa nyeti zinazopitia mnyororo wa huduma za posta. Katika zoezi hilo, Shirika la Posta Tanzania limepata alama 598 kati ya 640, likitimiza kwa ufanisi vigezo vyote vya kupewa cheti hicho cha heshima kinachotolewa kwa taasisi za posta zinazofikia viwango vya juu vya usalama wa kimataifa. Wakipokea cheti hicho, Caroline Kanuti kwa niaba ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, pamoja...