Posts

Showing posts from May, 2024

Wadau kuujadili uhuru wa habari Zanzibar

Image
NA MWANDISHI WETU KAMATI ya maandalizi ya siku ya uhuru wa habari duniani Zanzibar, imeeleza kuwa maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani yanategemewa kufanyika Mei 23, mwaka huu. Taarifa iliyotolewa kwa niaba ya kamati ya maandalizi ya maadhimisho hayo inayoundwa na Baraza la habari Tanzania (MCT ) Ofisi ya Zanzibar , Chama cha Waandishi   wa Habari Tanzania Zanzibar (TAMWA - ZNZ),  Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo (WAHAMAZA) na Klabu ya Waandishi wa Wabari Zanzibar (ZPC), Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk. Mzuri Issa, alisema  maadhimisho hayo yatafanyika ukumbi wa ZSSF Kariakoo Zanzibar. Alisema maadhimisho hayo yatahudhuriwa pamoja na waandishi wa habari, wadau mbali mbali wa habari na wawakilishi kutoka asasi za kiraia za ndani ya Zanzibar. Dk. Mzuri alisema kuwa maadhimisho ya mwaka huu yamebeba ujumbe wa ‘Uhuru wa vyombo vya habari na mageuzi ya sera na sheria za  habari Zanzibar’ ambao ni muhimu katika kukuza na kuimarisha kada ya ha...

TAMWA yawataka waandishi kuhimiza mabadiliko kijinsia michezoni.

Image
NA AMINA MCHEZO WAANDISHI wa habari wmeatakiwa kutumia kalamu zao kuwavuta na kuonesha fursa zilizopo Kwa wanawake michezoni. Akifungua mafunzo ya habari za jinsia na michezo kwa waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania  (TAMWA) Zanzibar, Dk. Mzuri Issa Ali katika ofisi za chama hicho Tunguu, mkoa wa Kusini Unguja. Amesema ushirikishwaji wa wanawake katika michezo ni mdogo kutokana na kutozungunzwa fursa katika vyombo vya habari. Amebainisha kuwa TAMWA kushirikiana na wadau mbalimbali wamesaidia kwa kiasi kikubwa kuondosha mifumo kandamizi kwa wanawake hasa katika nafasi za uongozi hivyo kwa sasa wameona kuna haja kuelekezwa nguvu michezoni. Kwa upande wake mkufunzi wa mafunzo hayo ambae pia ni Mjumbe wa bodi ya TAMWA Zanzibar, Hawra shamte amesema wanawake wana haki ya kushiriki katika michezo bila  ya kuvunja mila na tamaduni zao. Hawra amewatoa hofu wanawake wanaohitaji kushiriki katika michezo  na kusema wapo wanawake waliofan...

Wadau uwindaji kitalii wachangia miradi ya maendeleo

NA MWANDISHI WETU, ARUSHA UWINDAJI wa kitalii umechangia kiasi cha Dola 2,546,295 za Marekani sawa na Shilingi bilioni 6,606,635,525 ndani ya kipindi cha 2020/2021 na 2022/2023. Fedha hizo zimetolewa kwenye miradi mbali mbali ya maendeleo na uendelezaji na shughuli za uhifadhi kwenye Maeneo ya Hifadhi za Wanyamapori za Jamii (WMA). Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dunstan Kitandula, alieleza hayo alipokuwa anafungua warsha ya wadau wa uhifadhi wa mnyama tembo kwenye mifumo ya ikolojia inayovuka mipaka ya nchi jijini Arusha. Aidha Kitandula alisema kuwa pamoja na mchango mkubwa unaotolewa na uwindaji wa kitalii kwenye mifumo ikolojia inayovuka mipaka ya nchi, ipo haja ya kuchanganua changamoto za matumizi ya wanyamapori hao zinazochangiwa na wanyama hao kupatikana katika mifumo ya ikolojia inayovuka mipaka ya nchi hivyo tembo hutoka nchi moja kwenda nchi nyingine. Kitandula aliongeza kuwa katika warsha hiyo anategemea kuwa wadau mbalimbali wa uhifadhi watapata fursa ya kujadiliana c...