Maalim Seif: Viongozi tendeni haki kwa wote


NA MWANDISHI WETU

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amewata viongozi kutenda haki kwa Wazanzibar wote bila ya kujali tofouti zao.

Alisema kama wananchi na viongozi wao watashirikiana itakuwa chachu ya kusukuma mbele gurudumu la maedeleo miongoni mwa Wazanzibari.

Maalim Seif alisema hayo katika msikiti wa Jumuiya ya Waarabu, Rahaleo Unguja, alipoungana na waumini wa dini ya Kiislam kkatika swala ya Ijumaa.

Aliwataka viongozi waliochaguliwa na walioteuliwa kupiga vita ubaguzi wa aina yoyote katika kuwahudumia wananchi.

“Tukifanyakazi kwa pamoja nakuhakikishieni maendeleo ni rahisi sana,” alisema Malim Seif.

Sambamba na hilo amewataka waumini dini ya Kiislam kuiombea dua Zanzibar ili umoja uliopo udumu.

Akizugmzia kuhusu ajira uwepo wa utulivu ni muhimu kwa ushiriiana an sekta binafsi kuondoa changamoto ajira Viwani Zanzibar.

“Kama tukuvutana tutachelewa kupata maedeleo lakini sisi Wazanzibar tumelijua hilo ndio maana tukawa na Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alieleza Maalim Seif.

Alieleza kuwa changamoto ya ajira ni kubwa ambayo huipata wahitimu wa vyuo vya elimu ya Juu mbali mbali Tanzania.

Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga kutatua changamoto ya ajira inayowakabili kina mama na vijana na kuwataka wananchi wote kushiriki kwa hali na mali katika shuhuli za Maendeleo hapa nchini.

 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango