Taifa limepoteza kiongozi jasiri, mzalendo – Dk. Mwinyi

NA MWANDISHI WETU

MAKAMU wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, amefariki dunia.

Akitangaza kifo cha mwanasiasa huyo aliezaliwa Oktoba 22, 1943, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, alieleza kuwa Maalim Seif amefariki dunia jana katika hospitali ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

“Majira ya saa 5:26 asubuhi, makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad. Maalim amefariki wakati akiendelea na matibabu katika hospitali ya muhimbili alipokuwa amelazwa tokea tarehe 9 mwezi huu,” alieleza Dk. Mwinyi katika taarifa yake kupitia televisheni ya Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC).

Aidha Dk. Mwinyi alitoa pole kwa familia ya marehemu, viongozi na wanachama wa chama cha ACT Wazalendo, wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla akiwataka kuendelea kuwa watulivu na wavumilivu.

Maalim seif ambae hadi mauuti yanamkuta alikuwa mwenyekiti wa chama cha act wazalendo, alikuwa ni miongoni mwa wanachama na viongozi waanzilishi wa chama cha wananchi CUF mwaka 1992.

Aidha kiongozi huyo, aliekihama chama hicho machi 18, 2019 na kujiunga na ACT Wazalendo, aliasisi maridhiano ya kisasa ya Zanzibar yaliyoapelekea mabadiliko ya 10 ya katiba ya Zanzibar ya 1984 yaliyoanzisha serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar.

Baada ya kutolewa kwa tangazo hilo, viongozi na wananchi mbali mbali walijitokeza na kutoa salamu za pole kwa familia, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Watanzania na Wazanzibari.

Miongoini mwa viongozi hao ni rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, aliemtaja marehemu kuwa ni miongoni mwa viongozi wazalendo na kumuombea dua kwa mwenyezi mungu.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Maalim Seif Sharif Hamad. Natoa pole kwa Dk. Mwinyi, familia, Wazanzibari na Watanzania wote. Mungu amweke mahali pema, aamini,” alieleza Dk. Maguli katika ukurasa wake wa ‘twitter’.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango