Dk. Mkuya ahimiza uwajibikaji taasisi zilizo wizarani kwake
RAYA HAMAD, OMKR
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Dk. Saada Mkuya Salum, amewataka watendaji na wafanyakazi wa Tume ya Kuratibu na Udhubiti wa Dawa za Kulevya, kuongeza juhudi zamapambano dhidi ya wanaoingiza, kuuza na kusambaza kwa maslahi ya Zanzibar
Dk. Saada ameeleza hayo alipokutana na uongozi na wafanyakazi wa tume hiyo
na kuwasisitiza kuwa waadilifu na waaminifu kwa vile ya matumizi ya dawa za
kulevya ni kero katika jamii na mtandao wake ni mkubwa
Ameeleza kuwa katika kusimamia vyema utekelezaji wa majukumu ya tume hiyo
Dk. Saada, amewataka kuzidisha
mashirikiano na taasisi mbalimbali wanazofanya kazi kwa ukaribu ikiwemo Uwanja
wa ndege, Bandarini, kikanda, kitaifa na
kimataifa na kusambaratisha mitandao wa wahalifu
Pia amewakumbusha kuwa hivi sasa fursa nyingi za maendeleo zinapatikana
zikiwemo utalii ujenzi wa miundo mbinu ambazo zimekuwa zikiibua fursa mbali
mbali za kiuchumi na kuiwa na
maingiliano jambo ambalo wahalifu wa madawa ya kulevya nao hugeuza fursa kwa
upande wao na kutumia mwanya huo kuingiza madawa ya kulevya
Aidha waziri huyo amewahimiza
watendaji kuvitumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kufikisha elimu
kwa wananchi pamoja na kufanya tathmini juu ya kile wanachokitoa hatua ambayo
itasaidia kufahamu mapungufu yaliyopo kwa upande wao
Amesema atahakikisha anashirikiana na watendaji na anasimamia vyema sheria na sera ikiwemo kuzipitia upya na kufanya marekebisho
pale panapohitajika kufanya hivyo ili kuwabana wahalifu na kuifanya jamii na
Serikali iwe huru
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa tume hiyo, Kheriyangu Mgeni Khamis,
amesema pamoja na mambo mengine tume imefanikiwa kuteketeza dawa za
kulevya kitaalamu , kuanzishwa kwa nyumba za kurekebisha tabia, kufanya
marekebisho ya Sheria 2019 na kubadilisha vifungu vya adhabu, kuimarisha
mashirikiano ya kitaifa na kimataifa
Ameeleza kuwa kupungua kwa
unyanyapaa kwa wanaochana na matumizi ya dawa za kulevya, kubadilika na
kukubalika kwa familia zao ambao awali waliwakataa kutokan na tabia ya matumizi
ya dawa za kulevya
Wakati huo huo Dk. Saada, ametembelea ofisi za Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC)
na kuwaomba watendaji wa tume hiyo kuharakisha utoaji wa muongozo na kufanyiwa
kazi, ikizingatiwa kuwa watendaji wakuu wengi ni wapya ili wapate fursa ya
kuupitia
Amesema pamoja na kuwa ZAC kujitihidi kutoa elimu, bado kuna haja ya
kutilia mkazo kwa baadhi ya maeneo korofi, taasisi za wafanyakazi sehemu za
utalii na kwengineko ili kuepusha maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi pamoja
na kuwaandalia mazingira bora ya watu wanaoishi na virusi hivyo.
Amewataka watendaji wasiridhike na kiwango cha maambukizi cha sasa cha
asilimia 0.4 kwa vile maaingiliano ni makubwa hasa kwa wakati huu ambao
Zanzibar inapata wageni wengi aidha matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii nayo
inachochea masuala ya kujamiiana hasa kwa vijana
Nae Mkurugenzo Mtendaji wa Tume ya Ukimwi, Dk. Ahmeid Mohammed Khatib
Reja, amesema moja kati ya mafanikio ya tume ni jamii imeelimika na hivyo
kupunguwa kwa unyanyapaa, tokea ukimwi ulipoingia Zanzibar haijawahi kuvuka
kiwango cha asilimia 1 ukilinganisha na mataifa mengine ambapo kiwango huwa
juu.
Hata hivyo ameelezea changamoto na matarajio tume hio ambapo amesema
kuongezeka kwa tabia hatarishi na matendo maovu ya udhalilishaji kama ubakaji
na kujamiiana kusiko salama bado ni changamoto
Aidha alieleza kuwa tume imejipanga kuzijengea uwezo baadhi ya Shehia
zilizoko ukanda wa pwani ambako utafiti wao wameona haziko salama kutokana na
maingiliano na watu wenye mazingira na tabia tofauti ili vijana na wazee waweze
kufahamu mazingira hatarishi na namna ya kukabiliana nazo.
Comments
Post a Comment