RoAID yazipatia manispaa gari za kubebea taka

NA MWANDISHI MAALUM

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imeeleza kuwa inathamini mchango wa taasisi za kimataifa na washirika wa maendeleo kwani unachochea kasi ya maendeleo ya nchi na ustawi wa jamii.

Kauli hiyo imetolewa na waziri wan chi, ofisi ya rais, tawala za mikoa na idara maalum za SMZ, Masoud Mohammed Ali, wakati akizungumza katika hafla ya kupokea magari manne ya kubebea takataka yaliyotolewa na serikali ya Romania kupitia Shirika la Misaada la nchi hiyo (RoAID).

Alisema msaada huo umekuja wakati muafaka kwa kuzingatia kuwa serikali ya awamu ya nane imeweka mkazo na kipaumbele katika usafi wa mji, hivyo msaada huo utaoingeza kasi ya udhibiti na uondoaji wa taka katika manispaa na halmashauri za miji ya Zanzibar.

Alifafanua kuwa swala la uchafu wa mji limekuwa kero ya muda mrefu na kupigiwa kelele na viomngozi wakuu wa nchi hivyo kuna haja ya watendaji wa manispaa kuongeza kasi ya usafishaji wa miji.

“Ikifika mahali hata kiongozi mkuu wa nchi (Rais) anaonesha kutoridhika na kazi mnazozifanya,viongozi na watendaji wa manispaa pamoja na halmashauri mnapaswa kujitathmini lakini pia kujiwekea malengo katika utendaji na usimamizi wa utekelezaji wa majukumu yenu,” alisema Masoud.

Waziri huyo aliishukuru kampuni ya Rom Solutions ya Zanzibar na Premium Audit kwa kufanikisha upatikanaji wa magari hayo jambo ambalo ni mwendelezo wa misaada inayotolewa na taasisi hizo katika litaongeza ufanisi katika

“Rafiki wa kweli utamjua wakati wa shida, ninazo taarifa kwamba msaada wenye mnasaba na huu ulitolewa kwa manispaa na halmashauri zote za Zanzibar, ndio maana ninawapongeza Rom Solutions na Premium Audit kwa kuratibu upatikanaji wa msaada hii,” alieleza Masoud.

Aidha waziri masoud aliwataka madereva na viongozi wa manispaa zitakazotumia gari hizo, kuzitunza ili msaada huo uwe na tija.

Mapema akitoa taarifa fupi ya msaada huo, mtendaji mkuu wa taasisi ya Premium Audit, Any Ivan – Vasilica, alieleza kuwa magari hayo ya kisasa yametolewa msaada na shirika hilo kwa watu wa Zanzibar ili kuunga mkono juhudi zinazochukuliwa na serikali kuimarisha usafi wa mji.

Alisema licha ya juhudi zinazofanya na taasisi zinazohusiana na usafoishaji wa miji, bado hali ya udhibiti wa takataka umekuwa na changamoto jambo ambalo linahitaji mchango wa kila mmoja.

“Toka tumeanza kufanya kazi Zanzibar mwaka 2018, wakati wote kipaumbele cha kwanza ni mambo yanayoihusu jamii ya Zanzibar tukiamini kuwa na sisi ni sehemu yake,” alisema Any.

Alisema shirika la RoAid litaendelea kutoa mchango wake kwa taasisi na serikali ya Zanzibar na kushukuru ushirikiano inayoupata katika utekelezaji wa majukumu yake.

Akimkaribisha mgeni rasmi, Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Zanzibar, Said Salmin Ufuzo, alieleza kuwa gari hizo zenye uwezo wa kukusanya takataka zitatolewa kwa manispaa tatu za unguja na moja ya pemba ili kuongeza kasi ya uwekaji mji katika hali ya usafi.

Alizitaja manispaa zitakazonufaika na msaada huo kuwa ni manispaa ya Mjini, Manispaa ya Magharibi ‘A’ na Magharibi ‘B’ kwa Unguja na Baraza la Mji Chakechake Pemba.

“Tunaamini magari haya yataongeza ufanisi katika shughuli za uzoaji wa takataka kutoka katika vituo vya kukusanyia na kuzipeleka jaa kuu Kibele,” alieleza Ufuzo.

Katika hafla hiyo iliyofanyika katika ofisi za Rom Solution Kisauni wilaya ya Magharibi ‘B’, madereva waliopewa mafunzo walikabidhiwa vyeti na funguo za magari hayo yaliyogharimu jumla ya Euro 160,000 zilizotolewa na shirika la RoAid.

Comments

Popular posts from this blog

'Zanzibar Matibabu Card' yashinda tuzo ya WSIS

ZAMECO yakerwa na video ya udhalilishaji mtandaoni

ZAMECO yakumbushia sheria mpya ya habari