Soraga ahimiza mafunzo kwa watendaji kuongeza ufanisi 

NA SHARIFA MAULID, WNARKUU

WAZIRI wa Nchi Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mudrik Ramadhan Soraga, ametilia mkazo suala la kupatiwa mafunzo wafanyakazi ili kuwajengea uwezo wa utakaoimarisha utendaji katika maeneo yao.

Ameeleza hayo wakati akizungumza na wafanyakazi wa Idara ya Utumishi na Uwendeshaji ya wizara hiyo juu ya utekelezaji wa majukumu  yao katika ukumbi wa wizara yake Mwanakwerekwe, wilaya ya Magharib ‘B’.

Alisema katika utekelezaji wake, Wakurugenzi wa idara hiyo waangalie mahitaji na sio kupewa mtu mmoja kila inapotokea nafasi za mafunzo ili kuondosha manung’uniko miongoni mwa wafanyakazi.

Soraga aliwataka viongozi na wafanyakazi kufuata taratibu za kazi, muongozo  wa sheria za kazi na maagizo yanayotolewa na serikali kwa lengo la kuweka mustakabali mzuri utaopelekea ufanisi wa majukumu  ya kila mmoja na maendeleo ya wananchi kwa ujumla.

Hivyo aliutaka uongozi wa Idara hiyo kuhakikisha wafanyakazi wanapatiwa stahiki zao, kupandishwa madaraja na kuweka mfumo mzuri utakaoweka wazi kujua muda wa kuingia na kutoka kazini kuimarisha nidhamu kazini.

“Tukiweza kufanikisha haya, sina shaka tutafika mbali na kwa ufanisi kwani sisi sote tunafanyakazi moja, tushirikiane, tuwe na mawasiliano mazuri na kuzidisha umoja wetu,” alisema Mudrik.

Aidha Soraga alisisitiza haja ya kutumiwa kikamilifu anuani za barua pepe za wizara katika mawasiliano ya kikazi badala ya kutumia barua pepe binafsi kwani kufanya hivyo kunavujisha taarifa za serikali.

“Hakikisheni wafanyakazi wote mnawapatia email zao za Wizara hili si ombi ni amri, tuna mambo mengi ya serikali, sasa kutumia e-mail (barua pepe) binafsi, hii ni kurahisisha uvujaji wa taarifa za serikali,” alieleza waziri huyo.

Katika hatua nyengine, Soraga aliwataka watendaji wa idara hiyo kuwa makini katika utendaji wa kazi zao na kukemea tabia ya baadhi ya watumishi kuondoka kazini kabla ya wakati.

Kuhusu wakurugenzi wa Idara zilizomo katika wizara yake, Soraga aliwataka kutumia vyombo vya habari wanapofanya shughuli zao ili wananchi wajue serikali inayoyafanya.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango