Vijana
watakiwa kutumia vyema mitandao ya kijamii
NA
MADINA ISSA
MKURUGENZI
Mtendaji wa Jumuiya wa Jukwaa la Vijana Zanzibar Zanzibar Youth Forum (ZYF), Maulid
Suleiman, (pichani aliesimama) amewataka vijana nchini kutumia mitandao ya kijamii ipasavyo, ili
kuepusha kuleta athari kwa mbalimbali kwa jamii.
Maulid
alitoa wito huo jana wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo vijana kupitia
mradi wa kukuza ushiriki wa asasi za kiraia katika sheria na uhuru wa msingi wa
vyombo vya habari, yaliyofanyika katika ukumbi wa kitengo cha kudhibiti malaria
Mwanakwerekwe Mjini Unguja.
Alisema
vijana wengi wanatumia vibaya mitandao hiyo na kusababisha migogoro ndani ya
jamii.
Alisema
ni vyema kwa vijana hao kutumia mitandao hiyo kwa kutoa taarifa sahihi ambazo
zitaleta mafanikio nchini na kufikia malengo yaliyokusudiwa ikiwemo kuelimisha
jamii hasa wanaotumia mitandao ya kijamii.
Aidha
alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuwajengea uwezo taasisi zisizo za
kiserikali na ushiriki na utetezi juu ya sera za habari, uhuru wa habari na
haki za msingi za binaadamu.
Akiwasilisha
mada ya matumizi ya mazuri ya mitandao, Mwanahabari Mwandamizi, Dk. Suleiman Seif
Omar, alisema wapo baadhi ya vijana hutumia mitandao ya kijamii kwa kuandika
taarifa bila ya kufuata sheria jambo ambalo linaweza kuleta vurugu na sintofahamu
katika nchi.
alisema
kupatiwa mafunzo hayo kutawawezesha kutangaza habari zilizokuwa na ubora na za
kweli kwa lengo la kuielimisha jamii.
“Sasa
hivi kila mtu ni muandishi wa habari watu wanaitumia taaluma hii wanavyotaka
hivyo ni vyema vijana wakaacha mtindo huu kwani uandishi wa habari ni taaluma
na unatakiwa usome na kujua taratibu za kupasha habari na sio uvamie tu,”
alisema.
Hivyo,
alisema ni vyema wakatumia taratibu na sheria za mitandao ya kijamii kwa
kuandika taarifa bila ya kumkwaza mtu kwa kutuma picha sahihi na taarifa
zilizokuwa sio za uongo ambazo zitakuwa zimefanyiwa tafiti wa kina ili kuweza
kufaidia juu ya habari atakayoituma.
Nao,
baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, walisema mafunzo hayo yatawasaidia kujua
sheria za mitandao na kutoa taarifa sahihi kupitia mitandao au mawasiliano yao
ya kawaida.
Walisema
ipo haja kwa asasi za kiraia kutumia mitandao ya jamii kuimarisha upatikanaji
wa habari kwa jamii ili kustawisha maendeleo ya nchi na watu wake.
Mradi
huo wa miaka miwili, unatekelezwa na ZYF chini ya ufadhiliwa na shirika la
International Media Support (IMS) la Denmark chini ya uangalizi wa MISA TAN,
UTPC na TAMWA umelenga kuimarisha matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii na
kuongeza uelewa wa wanachama wa asasi za kiraia juu ya sheria zinazohusiana na
vyombo vya habari.
Comments
Post a Comment