Waziri ataka wanawake kuinua sekta ya utalii

NA MWANDISHI WETU

WAZIRI wa Utalii na Mambo ya Kale, Lela Mohammed Mussa, amewataka wanawake kuungana kuitetea jinsia yao na kuachana na mila za kuamini kuwa kufanya kazi katika sekta ya utalii kwa wanawake ni kinyume na utamaduni.

Akizungumza katika hafla ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Machi 8, mwaka huu iliyoandaliwa na hoteli ya Park Hyatt, ikiwa na lengo la kuwahamasisha wanawake kuunga mkono katika shughuli mbali mbali zikiwemo za kisiasa na kijamii.

Alisema jamii ya Wazanzibari imekuwa ikitawaliwa na dhana mbaya kuhusiana na sekta hiyo kiutalii lakini jamii hiyo ya wanawake inajitambua na imeonekana kufanya vizuri katika ajira mbali mbali bila ya kuharibu mila, silka, desturi na tamaduni zao.

Aidha alisema utafiti uliofanyika duniani unaonesha kuwa dhamana nyingi walizopewa wanawake kuzifanyia kazi wamekuwa wakifanya vizuri zaidi kuliko wanaume.

Hivyo, alisema kuwa hakuna haja ya kuendelea kuvunjana moyo na badala yake wawe kitu kimoja hasa Katika kuendelea kuleta mabadiliko Katika nchi.

Naye Meneja Mkuu wa hoteli ya Park Hyyat, Nicolas Cedro, alisema hoteli hiyo inathamini utendaji wa kazi kwa jinsia ya kike kwani wamekua na mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa nchi.

"Katika hoteli yetu tumekuwa tukithamini sana wanawake, kwani wana mchango mkubwa sana katika kufanya kazi na siye tutaendelea kuwathamini na kujua umuhimu wa kazi zao wanazozifanya," alisema.

Mapema Mejeja Rasilimali watu katika hotel hiyo, Catherine Msuya, alisema atahakikisha wanaongeza nafasi kwa wanawake ambao kwa sasa ni zaidi ya asilimia 20 ya wafanyakazi wote hotelini hapo.

PICHANI:

WAZIRI wa Utalii na Mambo ya Kale, Lela Mohammed Mussa akipokea cheti cha shukran kutoka kwa Meneja Mkuu wa hoteli ya Park Hyyat Nicolas Cedro Wakati wa sherehe za maadhimisho ya siku wa wanawake Machi 8 mwaka huu. Wa kwanza kulia ni afisa rasili mali watu wa hoteli hiyo, Catherine Msuya. (PICHA NA MZEE GEORGE).

 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango