ZPC yaomboleza kifo cha JPM
NA MZEE GEORGE
WAKATI mwili wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, marehemu Dk. John Magufuli ukifikishwa katika kijiji chao cha Chato
mkoani Geita, wananchi na viongozi wa ngazi mbali mbali wamejitokeza kusaini
vitabu vya maombolezo vilivyowekwa katika maeneo mbali mbali nchini.
Miongoni mwa wananchi na viongozi waliofanya
hivyo jana ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein
Ali Mwinyi, alieweka saini katika vitabu hivyo vilivyowekwa katika Ofisi Kuu ya
CCM Zanzibar Kisiwandui na ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil.
Kwa upande wa viongozi wa asasi za kirai, Katibu
Mkuu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar, Mwinyimvua Nzukwi ambae aliweka saini katika vitabu hivyo Machi 24, 2020 na kueleza kusikitishwa kwao na kifo hicho.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Nzukwi
alieleza kuwa kifo cha Dk. Magufuli ni pigo na kwamba kimeacha pengo katika
ujenzi wa taifa.
Alieleza kuwa Dk. Magufuli licha ya kuwa ni
kiongozi wa kitaifa, bado alikuwa mdau na chanzo muhimu cha habari na
kuvipongeza vyombo vya habari kwa kuungana na kutoa taarifa za matukio ya kifo
cha kiongozi huyo.
Alisema toka kutokea kwa msiba huo, vyombo vya
habari vimekuwa vikitoa taarifa na uchambuzi wa habari uliowawezesha watanzania
na walimwengu kuwa na uelewa jambo lilisaidia kuongeza umoja na mshikamano kama
taifa.
Akizungumzia hatua ya kusaini kitabu hicho
alisema kunatokana na kuguswa kama mwananchi lakini kiongozi wa taasisi
inayowaunganisha waandishi, waliona umuhumu wa kuonesha kuhguswa kwao na kifo
cha kiongozi huyo aliefariki Machi 17, 2021 katika hospitali ya Mzena jijini Dar
es salam.
“Hakika umeondoka wakati sote tukikuhitaji, pumzika
kwa amani. RIP – JPM,” aliandika Nzukwi katika kitabu cha CCM na “Waandishi wa
habari na Wanachama wa Klabu za Wanahabari zitakumbuka mchango wako katika
ujenzi wa taifa siku zote, RIP – JPM,” katika kitabu cha serikali.
Maziko ya Dk. Magufuli yanatarajiwa kufanyika
machi 26, 2020 kijijini kwao chato, mkoani Geita ambapo mwili wa kiongozi huyo
ulifikishwa kijijini hapo Machi 24, 2021 majira ya saa 12:30 jioni ukitokea Zanzibar
ambapo uliagwa Machi 23 kabla ya kuagwa Mwanza asubuhi ya Machi 24, 2021.
Pichani na maelezo:
Comments
Post a Comment