Ayoub ahimiza upatikanaji wa habari sahihi

NA MWAJUMA JUMA

MKUU wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Ayoub Mohammed Mahmoud, ameeleza kuwa upatikanaji kwa habari sahihi na kwa wakati ni jambo la lazima hivyo wanahabari wanapaswa kwenda na kasi ya ukuaji wa teknolojia ya habari na mawasiliano.

Ayuob aliyasema hayo alipokutana na wajumbe wa Kamati Tendaji ya Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), waliyofika ofisini kwake kujitambulisha huko ofsini kwake Mkokotoni mkoani humo.

Alisema kutokana na mabadiliko ya teknolojia, jamii imekuwa ikipata habari nyingi ambazo baadhi yao sio sahihi na kupelekea athari kwa jamii na ikiwemo migogoro na machafuko ya kijamii.

“Kwa tulipofikia, swala la kupatikana kwa habari sahihi ni jambo la lazima kwani zinapokosekana habari sahihi hutolewa sizizo sahihi na zinapoifikia jamii athari yake inakuwa kubwa na tunaweza kupelekea nchi ikaingia kwenye migogoro ikiwemo ya kivita”, alisema.

Hivyo alisema uwepo wa Klabu ya Waandishi wa Habari ni faraja kwa sababu ni chombo ambacho kinakwenda kuiunganisha tasnia ya habari na hatimae kuwanganisha wale wataalamu wenyewe wakaweza kufanya kazi kwa uweledi na ufanisi.

Alisema kuwa dhamira ya kuanzishwa kwa chombo hicho ni kuendeleza tasnia ya waandishi wa habari, ambayo ni muhimu kubwa katika utoaji wa taarifa kwa jamii.

Sambamba na hayo alisema kuwa akiwa yeye ni mlezi wa taasisi hiyo ana kila sababu ya kuona kwamba programu ambazo zilisita zinafanyiwa utaratibu wa kufanyika.

“Nikubaliane na nyinyi kwa sasa kwamba tuna kila sababu ya kuona zile programu ambazo zinaweza kutekelezeka kwa sasa zinafanyika,” alisema.

Aidha alisema kuwa programu ya kufundisha uchumi wa bluu ni programu nzuri na wa mkoa walitoa tangazo ambalo lilizungumzia dhana ya uchumi huo na namna ya  kuweza  kummunga mkono rais wa Zanzibar lakini pia waweze kuifahamu na kuiishi na kuifaidi.

Hivyo alisema dhana hiyo wao wameitafasiri katika  tamasha moja linaloitwa tamasha la Vyakula vya Pwani Zanzibar , ‘Zanzibar Sea Food Festival’, ambapo alisema kupitia tamasha hilo anaamini kuwa wadau wanaoamini uchumi wa buluu wa moja kwa moja na wasio moja kwa moja watafikiwa na kuunganishwa.

“Kwa hiyo nanyi mutakapokuja kujifunza dhana ya uchumi wa buluu na sisi tutapata nafasi ya kuwasilisha hoja yao juu ya tamasha hilo kwa mkoa wao ili waandishi mukaweza kuibeba na kuipeleka mbali zaidi”, alisema Ayoub mbele ya Katibu Tawala wa mkoa huo Makame Machano Haji.

Alieleza kuwa anaamini kupitia dhana hiyo na kupitia sera hiyo ya taifa sasa wananchi walio wengi wataweza kupata tija na maslahi yaliyo makubwa zaidi kukuwa kwao kiuchumina ustawi wa jamii kupitia dhana ya uchumi wa buluu.

Aidha alivipongeza vyombo vya habari vya Zanzibar kwa jinsi vinavyofanya kazi ya kushajihisha umoja na ushirikiano wa jamii hasa wakati wa msiba wa aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania marehemu Dk. John Pombe Magufuli.

Awali Mwenyekiti wa klabu hiyo Abdalla Abdulrahman Mfaume na Katibu Mkuu Mwinyimvua Nzukwi, walimueleza mkuu huyo wa mko kwamba klabiu hiyo imejipanda kuwaendeleza wanachama wake katika aina mbali mbali za uandishi ili kukuza weledi.

“Kwa mfano katika robo ya kwanza ya mwaka tulipanga nkuwafundisha wanachama wetu namna ya kuzitambu, kuziibua na kuandika habari za uchumi wa buluu tukiamini kwamba watakapoielewa kwa kina dhana hii, watawasaidia wananchi kunufaika nao,” alieleza Mfaume.

Aidha Mwenyekiti huyo alisema ziara hiyo ni kawaida kwa kiongoizi huyo ambae ni Mlezi wa jumuiya yao, aliahidi kuendelea kushirikia nan a kiongozi huyo na watendaji wake ili kuhakikisha mafanikio ya pande zote mbili yanapatikana.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango