Mbunge Welezo akemea udhalilisahaji watu wenye ulemavu

NA MWANDISHI WETU

WAZAZI na walezi wenye watoto wenye ulemavu, wameombwa kutowaficha kwani kufanya hivyo ni sehemu ya udhalilishaji na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Wito huo umetolewa na Mbunge wa jimbo la Welezo, Unguja katika hafla ya kukabidhi viti mwendo (wheel chair) kwa watu wenye ulemavu wa jimbo hilo iliyofanyika katika tawi la CCM Mwendapole, shehia ya Welezo wilaya ya Magharibi ‘A’.

Alieleza kuwa kushirikishwa kwa watu wenye mahitaji maalum katika shuguli za kijamii ni miongoni mwa haki za binadamu hivyo ipo haja ya elimu iendelee kutolewa.

“Watu wenye ulemavu na wenye mahitaji maalum ni sehemu ya jamii, hivyo tuwatoeni na kuwapeleka skuli ili kupata elimu lakini pia tuwashirikishe katika mambo mengine ya kijamii,” alisema Maulid.

Aidha aliwapongeza wananchi wa jimbo hilo kwa mashirikiano wanayoyatoa kwa viongozi wa jimbo hilo jambo linalopelekea utekelezaji wa ilani ya uchaguzi kwa ufanisi.

“Tuendelee kushikamana na kushirikiana ili tuweze kukamilisha utekelezaji wa ilani ya CCM na mipango ya nchi yetu kwa wakati,” alieleza Maulid.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, mzee Usinga Makame Suha, alimshukuru kiongozi huyo na kueleza kuwa kiti hicho kiamsaidia mtoto wake kujumuika na wenziwe katika masomo na michezo.

“naomba wazazi wenzangu wasione kuwa na motto mwenye ulemavu kama ni mkosi, tuwape nafasi ya kusoma tusiwafungie ndani,” alieleza usinba baba wa rauhiya.

Nae mzazi wa mtoto Muayar Mussa Ali, aliiomba serikali kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili iwalinde watoto wenye ulemavu dhidi ya aina zote za udhalilishaji.

“Kuwaficha ndani watu wenye ulemavu kwa kuogopa aibu ni udhalilishaji ambao unapaswa kukemewa ili kuuondoa ndani ya jamii,” alisema Mussa.

Awali akitoa maelezo juu ya shughuli hiyo, Katibu wa CCM jimbo la Welezo, Mwanakhamis Khamis Idi, aliwapongeza viongozi wa jimbo hilo kwa kuanza kutekeleza ahadi zao na kuwaomba waendelee kufanya hivyo katika makundi na maeneo mengine ya jamii.

“Wakati wa kampeni zipo ahadi zilitolewa na viongozi kama ahadi zao, ninashukuru kwamba umeanza kutekeleza ahadi hizo na kukijengea uaminifu chama chetu,” alisema Katibu huyo.

Jumla ya shilingi milioni 8.5 zimetumika kununulia viti hivyo vilivyotolewa kwa watoto na watu wazima wenye ulemavu wa viungo vya miguu na mwili ili kuwaondolea changamoto ya usafiri kutoka sehemu moja na nyengine.

 

 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango