Wanahabari wahimizwa ‘kuilea’ SUK

NA MWAJUMA JUMA

MKURUGENZI wa Chama Cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania (TAMWA) ofisi ya Zanzibar, Dk. Mzuri Issa amesema kunahitajika nguvu ya pamoja ili kuimarisha maridhiano ya kisiasa yaliyoasisi Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) Zanzibar.

Akizungumza katika mafunzo ya Waandishi wa habari juu ya umuhimu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa, alisema waandishi wa habari wanapaswa kuchukua jukumu lao na kuhakikisha lengo la kuanzishwa kwake linafanikiwa.

Alisema kwenye taifa, ustawi na umoja wa wananchi ni nguvu kubwa katika kuhakikisha maendeleo yanapatikana.

Hivyo alieleza kuwa waandishi wa habari wana wajibu wa kuacha ushabiki wa siasa bali wajuwe kwamba wao ndio wanaopaswa kupaza sauti zao ili jamii izidi kujenga matumaini na serikali hiyo.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo, Mkufunzi wa Waandishi kutoka Internews, Ali Haji Mwadini, alisema pamoja na waandishi kufanya kazi katika mazingira magumu, bado wanajukumu la kuifahamisha jamii hasa wa vijijini kuhusu Serikali hiyo.

Hata hivyo alisema kuwa kufa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya 2010 kulichangiwa sana na waandishi wa habari ambao hawakuweza kutimiza majukumu yao katika kuihamaisiha jamii juu ya uwepo wake.

Hivyo alisema ili wasirejee nyuma ni wajibu wao sasa kutumia kalamu zao kwa kuandika mara kwa mara SUK, ambayo wananchi wanaonekana wana matumaini makubwa na serikali hiyo. 

Wakichangia mada hiyo baadhi ya waandishi wa habari walisema kufa kwa serikali hiyo 2010 kulitokana na waandishi kuwa na woga, kuingiza utashi wa kisiasa pamoja na kutokujiamini juu ya kuandika habari ambazo zinahusiana na SUK.

Hata hivyo walisema pamoja na uwepo wa serikali hiyo lakini bado wanawoga kwa kuingiza mambo ya nyuma na wengi wao kudhani kwamba ndani ya Serikali hiyo kuna chama cha siasa.

Mafunzo hayo ya siku moja yaliandaliwa na Chama cha Wandishi wa Habari wanawake Tanzania (TAMWA) Zanzibar kupitia mradi wa kuwajenga kiwezo wanawake katika uongozi (SWIL) unaofadhiliwa na UN Women.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango