ZBS yataja chanzo kupanda gharama ukaguzi bidhaa

NA MWANDISHI WETU

TAASISI ya Viwango Zanzibar (ZBS) imeeleza kuwa gharama kubwa za kuthibitisha ubora wa bidhaa za wajasiriamali inatokana na kutokamilika kwa maabara ya upimaji wa bidhaa za vyakula ya taasisisi hiyo na mlolongo wa vipimo vinavyohitajika kufanyika.

Akizungumza na Waandishi wa habari huko Ofisini kwake Amani, Mkuu wa taasisi hiyo, Rahima Ali Bakari, ameitaja hatua hiyo hupelekea wajasiriamali wengi kushindwa kumudu gharama hizo na kupelekea malalamiko

y
a wajasiriamali kutokana na kutomudu gharama hizo.

Alisema kutokana na hilo, ZBS imeona haja ya kutafuta namna ya kuwasaidia wajasiriamali hao ili waedelee na kuzalisha bidhaa ikiwa ni pamoja na kuwapa ushauri juu ya namna ya kuvifikia vigezo na masharti ili kupata alama ya ubora wa bidhaa zao.

“Taasisi imeamua kuondoa gharama za ukaguzi na kuwashajihisha wawe na maeneo bora ya kufanyia shughuli zao lakini pia kuwaunganisha na mamlaka nyengine zinazoweza kuwasaidia kuvifikia viwango vya ubora,” alieleza Rahima.

Akizungumzia masuala ya vifungashio vya bidhaa za wajasiriamali, Rahima, alifahamisha kuwa watashauriana na taasisi husika ikiwemo Mamlaka wa viwanda vidogo na vya kati (SMIDA) ili kuwaendeleza.

Aidha alisema licha ya kuondolewa kwa gharama za ukaguzi lakini changamoto iliyopo ni gharama za upimaji wa viwango vya bidhaa za vyakula kutokana na kutokamilika kwa maabara ya upimaji wa bidhaa za vyakula ya taasisi hiyo.

“Gharama za upimaji hasa wa bidhaa za vyakula ni kubwa na ZBS inashindwa kuwasaidia wajasiliamali wote lakini pia wao wenyewe pia hawaziwezi ndio maana tumewaweka kwenye mpango kazi wetu wa mwaka ujao wa fedha,” alisema Mkurugenzi huyo.

Alieleza kuwa ili kufikia azma hiyo, ZBS imejipanga kuwatambua wajasiriamali hao na kuwaweka katika makundi maalum ili iwe rahisi kuwahiudumia ikiwa ni pamoja na kubeba gharama za upimaji kwa wale watakaokidhi  vigezo.

 “Kweli gharama kubwa na wajasiriamali hawaziwezi, kwa mfano kwenye bidhaa za vyakula, kipimo kimoja kinafika dola za marekani 50 na bidhaa inatakiwa ifanyiwe zaidi ya vipimo vitatu,” alieleza Rahima.

Hata hivyo aliwaomba wajasiriamali kuitumia taasisi hiyo kwa kupata ushauri wa kitaalamu ju ya uzalishaji wa bidhaa kwa lengo la kukabiliana na changamoto zilizopo ikiwemo ya kutokuwa na maeneo maalum ya kufanyia biashara zao hali inayopelekea hata ZBS kupata wakati mgumu wakati wa kufanya ukaguzi bidhaa zao.

Comments

Popular posts from this blog

'Zanzibar Matibabu Card' yashinda tuzo ya WSIS

ZAMECO yakerwa na video ya udhalilishaji mtandaoni

ZAMECO yakumbushia sheria mpya ya habari