DC Kunambi awaalika wananchi kukimbiza mwenge

NA SHADYA MOHAMED

MKUU wa wilaya ya Magharibi ‘A’, Suzan Kunambi amesema miradi mitano yenye thamani ya shilingi milioni 619,480 inatarajiwa kupitiwa na mwenge wa uhuru katika Wilaya hiyo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizo, Kunambi aliitaja miradi hiyo kuwa ni pamoja na mradi wa uhifadhi wa mazingira na miti asili uliopo katika shehia ya Kitundu.

Miradi mingine ni ya shamba darasa na bwawa la ufugaji wa samaki, kukagua huduma utoaji wa za afya ya kijiji, kuangalia darasa la TEHAMA na kituo cha kurekebisha taibia za watumiaji wa dawa za kulevya (Sober House).

“Maandalizi kwa ajili ya kuupokea mwenge wa uhuru ndani ya wilaya yetu yanaendelea vyema na ninawaomba wananchi wajitokeze kwa wingi ili zoezi la kuukimbiza mwenge lifanyike kwa ufanisi mkubwa,” alieleza Kunambi.

Mwenge wa uhuru ulioanza mbio zake Mei 17, 2021 katika mkoa wa Kusini Unguja, utaanza mbio zake katika mkoa wa Mjini Magharibi kupitia wilaya ya Magharibi ‘A’ kuanzia Mei 21, 2021 ambapo utakagua na kuzindua miradi mbali mbali.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango