Madiwani watakiwa kuchochea matumizi baraza watumiaji nishati

NA MWANAJUMA MMANGA

MADIWANI wa Mkoa wa Kaskazini Unguja wametakiwa kuwahamasisha wananchi kulitumia Baraza la Watumiaji wa Huduma za maji na nishati (CRC) kueleza matatizo yanayowakabili katika vijiji vyao kupitia sekta hizo.

Akitoa mafunzo kwa madiwani hao, Katibu Mtendaji baraza hilo, Hadia Abdulrahman Othman huko Mkokotoni, alisema lengo la serikali kuunda baraza hilo ni kulinda na kusimamia maslahi ya watumiaji kwa kuhakikisha matatizo yanayowakabili katika sekta za maji, umeme, mafuta na gesi yanapatiwa ufumbuzi. 

Aliwataka madiwani  hao kuzingatia taratibu zote za kisheria za uungaji na matumizi sahihi ya  huduma za maji na nishati ili ziwe endelevu na salama kwa wananchi.

“Niwaombe sana Madiwani kuhakikisha uungaji wa maji na nishati ya umeme unakuwa kwa mujibu wa sheria na akanuni zilizoekwa na serikali ili kuepusha kupotea kwa mapato ya seriakli sambamba na kuepusha malalamiko yanayojitokeza,” alieleza Hadia.

Hivyo aliwasihi wananchi kuacha tabia ya kujiungia kienyeji huduma hizo badala yake kufuata taratibu zilizowekwa na mamlaka husika ili kuondoa malalamiko yasiokuwa ya lazima.

Nao washiriki wa mafunzo hayo waliwaomba viongozi wa baraza hilo kuweka mawakala katika wilaya zote ili wananchi wapeleka malalamiko yao kwa urahisi kutokana na umuhimu wa huduma hizo.

“Sisi wananchi tutajitahidi kufata maelekezo ya kujiunga na huduma hizo na kufuata sheria zilizowekwa kwani hakutakuwa na vikwazo vyovyote vile na kuwataka wezetu kupunguza migongano baina ya ZAWA na ZURA,” walisema.

Mafunzo hayo ni sehemu ya utaratibu wa baraza hilo kujenga uelewa wa wadau wake na wananchi ili waweze kulitumia kutoa malalamiko kuhusiana na utendaji wa taasisi zinazojihusisha na utoaji wa huduma za maji, nishati ya umeme, mafuta na gesi asilia nchini.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango