Simai awataka walimu kutumia huduma za kibenki kujindeleza

NA HAROUB HUSSEIN

WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya AmaliZanzibar, Simai Mohammed Said, amewataka
walimu kuzitumia fursa zinazopatikana katika benki ya NMB ili kurahisisha upatikanaji wa mahitaji yao kwa maendeleo ya haraka.

Simai aliyaeleza hayo wakati akifungua semina ya Siku ya Walimu na NMB iliyofanyika katika ukumbi wa Michenzani Mall jijini Zanzibar.

Alisema benki ya NMB ina fursa mbali mbali zinazosaidia wafanyakazi katika mahitaji yao ya kila siku hivyo ni vyema walimu wakazitumia fursa hizo kujipatia maendeleo ya haraka.

Aidha alisema katika kujali watumishi wa wizara hiyo benki hiyo imeamua kuweka siku maalum ya walimu ikiamini walimu ndio msingi mkuu wa maendeleo katika sekta zote.

“Benki hii imeonesha kujali watumishi wetu kwa kuweka siku maalum ya walimu hivyo nakuombeni muwe karibu nayo kwa kuzitumia fursa na huduma zinazopatikana katika benki ya NMB,” alisema Waziri Simai.

Alisema katika kurahisisha huduma mbali mbali benki hiyo imekua ikitoa huduma hizo kwa njia ya mtandao wa simu na kufanya huduma zao kupatikana wakati wowote bila ya usumbufu.

Nae Meneja Mwandamizi wa NMB, Tito Mangesho alisema wamenzisha huduma ya NMB mkononi ambayo itawasaidia walimu katika maendeleo yao ya kila siku, hivyo amewashauri walimu hao kuzitumia ipasavyo fursa zinazopatikana katika benki hiyo kwa maendeleo ya leo na kesho.

Alisema nmb imekua na fursa mbalimbali ikiwemo ya mikopo ya nyumba kwa nyumba, bima pamoja na Sanlam life, hivyo aliwashauri walimu kuzitumia fursa hizo na nyenginezo ili kurahisha maisha yao.

Nae Meneja wa benki hiyo Kanda ya Zanzibar, Abdalla Duchi alisema benki hiyo ina zaidi ya wateja 2,500,000 nchini kote waliopo katika huduma ya kujihudumia wenyewe jambo lililopunguza misongamano ya wateja wanaofika ofisini.

Nao baadhi ya washiriki wa semina hiyo waliishukuru benki ya NMB kwa kuonesha kuwajali na kuwapa fursa zitakazowakwamua kimaisha.

Walisema mara nyingi walimu husahauliwa katika masuala mbali mbali ya maendeleo lakini benki hiyo imeamua kutenga siku maalum kwa walimu ikiwa ni ishara njema kwao ili waweze kutumia huduma hizo sambamba na kuinua maisha yao.

PICHA:


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Simai Mohamed Said (katikati) akimsikiliza MenejaMwandamini wa huduma za kidigitali kwa wateja wa benki NMB, Tito Mangesho katika mkutano wa siku ya walimu na NMB kwenye ukumbi wa Michenzani Mall mjini Zanzibar jana.



Meneja wa NMB klasta ya Zanzibar, Abdalla Duchi akitoa maelezo wakati wa mkutano wa siku ya walimu na NMB.


WALIMU kutoka skuli mbali mbali za Unguja waliohudhuria mkutano wa siku ya walimu na NMB kwenye ukumbi wa Michenzani Mall.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango