NMB yaipa Kusini Unguja msaada wa zaidi ya 25m/-

NA MWANDISHI WETU

MKUU wa Mkoa wa Kusini Unguja Rashid Hadid Rashid ameipongeza benki ya NMB kwa misaada mbali mbali wanayotoa kwa jamii hapa Zanzibar.

Alisema wananchi wa maeneo mbali mbali wamekuwa wakilalamikia changamoto za kijamii, ikiwemo sekta ya elimu kukosekana kwa madarasa ya kusomea baadhi ya madarasa kuvujisha hivyo misaada iliyotolewa na benki hiyo utasaidia kwa kiasi kikubwa kuondosha changamoto hizo.

Rashid alieleza hayo juzi wakati akipokea vifaa vya kuezekea skuli za mkoa huo na vitanda kwa ajili ya kujifungulia mama wajawazito ili kuwasaidia kwa namna moja ama nyengine.

Alisema msaada huo una thamani ya shilingi milioni 25 utatumika kuezekea skuli tatu kwa mkoa huo ikiwemo ya Kizimkazi, Makunduchi na Binguni.

“Serikali ya Mapinduzi imekua ikithamini na kutambua misaada inayotolewa na wadau wa maendeleo kama benki ya NMB kwani imekuwa ikisaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto za wananchi wetu,” alieleza Mkuu huyo wa amkoa.

Aidha Rashid aliipongeza benki hiyo kwa kuwa karibu na serikali na kuwasaidia wananchi wa Zanzibar wakiwemo wakulima wa mwani na wavuvi kwa kuzingatia sera ya Rais wa Zanzibar kuiendeleza sekta ya uchumi wa buluu.

Katika hafla hiyo iliyofanyika katika skuli ya Binguni, NMB pia ilikabidhi vitanda 12 kwa ajili ya vituo vya  afya vinavyotoa huduma za mama na watototo vya sehemu mbali mbali kikiwemo cha Mwera, Chwaka na Unguja Ukuu.

Aidha aliwaomba wananchi wa mkoa huo kutumia vyema inayotolewa na benki hiyo kuhusiana na programu inayojulikana wajibu ambapo inawafahamisha wanafunzi jinsiya kutumie na watunze fedha.

Rashid aliziomba taasisi nyengine kuiga mfano wa NMB na kutoa misaada mbali mbali itakayowanufaisha wananchikutatua changamoto za maji, barabara na masoko ili kukidhi mahitaji ya wananchi.

Kwa upande wake, Afisa  Mkuu wa  Wateja binafsi na Biashara wa NMB, Filbert Mponzi, akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo, alisema NMB hiyo imetoa msaada huo kama sehemu ya utaratibu wa benki hiyo kutenga  asilimia ya faida inayoipata kurejesha kwa wananchi.

Aidha aliahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuimarisha sekta mbali ya elimu na Afya katika mkoa wa Kusini Unguja ili kuhakikisha wananchi wanafaidika na huduma hizo.

Akitoa maneno ya shukrani, Awali Mkuu wa wilaya ya Kati, Marina Joel Thomas, aliishulkuru na kuipongeza NMB kwa kutoa msaada huo, ambapo aliwataka wasichoke kufanya hivyo ili kukoleza kasi ya maendeleo ya wananchi.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango