HAFLA YA UZINDUZI WA RASMI MWONGOZO WA MASHAURI KWA MAJAJI NA MAHAKIMU WANAWAKE KATIKA PICHA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akiondoa kitambaa kuzindua rasmi Mwongozo wa Mashauri kwa Majaji na Mahakimu Wanawake katika kutekeleza utoaji wa maamuzi na utendaji haki kwa familia, uliofanyika Oktoba 28, 2021 Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akikata utepe kuzindua rasmi Kitabu cha Mwongozo wa Mashauri kwa Majaji na Mahakimu Wanawake katika kutekeleza utoaji wa maamuzi na utendaji haki kwa familia. Uzinduzi huo umefanyika Oktoba, 28 2021 Ikulu Jijini Dar es Salaam. Kushoto Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi, wa pili kushoto Mwakilishi mkazi wa UN Women hapa nchini bibi.  Hodan Addou, kulia Balozi wa Sweden nchini, Anders Sjoberg na Mwenyekiti wa Chama cha Majaji na Mahakimu Wanawake (TAWJA) Jaji Joaquine De Mello.


Baadhi ya wanachama wa chama cha majaji na mahakimu wanawake (TAWJA) na waalikwa wengine wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa uzinduzi wa mwongozo wa mashauri kwa majaji na mahakimu wanawake katika utoaji wa maamuzi na utendaji haki kwa familia, Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Anders Sjoberg mara baada ya kuzindua rasmi mwongozo wa mashauri kwa majaji na mahakimu wanawake katika utoaji wa maamuzi na utendaji haki kwa familia, Ikulu Jijini Dar es Salaam. (PICHA NA IKULU).

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango