Samia awaapisha mawaziri, wajumbe NEC

  • LAwataka kuzingatia weledi, uwajibikaji

NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAM
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewaapisha viongozi mbali mbali aliowateua hivi karibuni na kuwataka kuzingatia weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Katika hafla hiyo iliyofanyika katika ikulu ya Dar es salam, Rais Samia amewaapisha viongozi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) pamoja na viongozi walioteuliwa kushika nafasi katika wizara ya habari na kuwaomba watekeleze majukumu yao kwa ufanisi.

Alisema uteuzi viongozi hao utaleta uwajibikaji mzuri hasa katika  sekta ya habari kwa vile hivi sasa inakwenda kwenye mabadiko ya kukuza matumizi ya teknologia.

Aidha aliwataka viongozi hao kuzingatia uwajibikaji na kusimamia utendaji kwenye maeneo yao ya kazi ili Tanzania ipige hatua za maendeleo kwa kasi zaidi.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Makamu wa Rais Dk. Isdori Mpango alisema imeonekana somo la aina ya uongozi anaoutaka Rais Samia halijaeleweka na Mawaziri na Makatibu wao na Mkatibu wakuu na Manaibu wake, kwani baadhi yao wanaendeleza mivutana ya kiutendaji.

Alisema hali hiyo haipendezi kuendelezwa na kuwaonya viongozi wenye tabia hiyo kuacha mara moja kwa kuwa Rais alishaonya hatolumbana na mtendaji yoyote ila atatumia kalamu yake kuchukua maamuzi.

Kutokana na hilo Makamu Mpango amesema akiwa yeye ndio msaidizi mkuu wa Rais anawaonya watendaji wenye tabia hiyo kwani hatoachia hali hiyo kuendelea kutokea.

Nae Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, alimpongeza Rais Samia kwa jitihada zake anazozifanya kwani kuna miradi mingi anayoitekeleza katika sekta mbali mbali ikiwemo ya michezo kwani imeonekana kufanya vizuri hivi sasa ndani  na nje ya nchi.

Alisema katika utekelezaji wa kazi za NEC, serikali haina wasiwasi kwani inafanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu ziliopo na kuahidi kuendelea kushirikiana nayo.

Akizungumza Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri, Dk. Tulia Akson, aliwata viongozi wa Tume ya Uchaguzi kufanya matayarisho ya uchaguzi mapema, badala kusubiri uchaguzi ufike, jambo ambalo wanasiasa wanatumia kuilalamikia tume ya uchaguzi  kutowatendea haki.

Katika hafla hiyo, Rais Samia alimuapisha Innocent Lugha Bashungwa kuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Pauline Philipo Gekul  kuwa Naibu Waziri wa wizara hiyo na Mhandishi Kundo Endrea Mathew kuwa Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Wajumbe wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Jacob Casthom Mwatembela Mwambengele, Magdalena Kamugisha Rwebangira, Asina Abdallah Omar .

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango