UN kusaidia utatuzi changamoto mifumo ya afya
NA MWANDISHI WETU
UMOJA wa Mataifa (UN) Tanzania umeeleza kuridhishwa na ushirikiano uliopo baina ya serikali za Tanzania katika kukabiliana na changamoto zinazoikabili jamii.
Hayo yameelezwa na watendaji masjhirika ya umoja huo katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ofisi za Umoja wa Mataifa Kinazini Zanzibar ikiwa ni miongoni mwa shughuli za maadhimisho ya miaka 76 toka kuasisiwa kwake.
Walieleza kuwa mashirika ya umoha huo, yanakusudia kushirikiana na serikali kuimarisha mifumo ya afya ili kuhamasisha jamii kuondokana na maradhi mbali mbali ukiwemo wa UVIKO 19.
Akizungumza
hatua hizo, Dk. Vendelin Simon kutoka Shirika la Afya Duniani (WHO), alisema
lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha ifikapo 2030 jamii inakuwa salama dhidi
ya magonjwa yakiwemo ya kuambukizia
“Kupitia maadhimisho haya tutajiikita zaidi katika kuimarisha mazingira ya usafi katika maeneo ya fukwe na kuyafikia makundi ya wanajamii wakiwemo wanafunzi kwa kuwapatia elimu ya kujikinga na magonjwa na majanga yakiwemo UVIKO 19 kwa kudumisha usafi muda wote,” alieleza Dk. Vendelin.
Nae Amina Kheir, kutoka Shirika la Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), alisema, wakati dunia inaendelea na mapambano dhidi ya UVIKO 19, UN itaendelea kuimarisha huduma za kinga na tiba hasa ikizingatia kuwa Zanzibar ni miongoni mwa nchi zinazopokea wageni kutoka mataifa mbali mbali.
“Sote tunaelewa kwamba kuzuka kwa maradhi haya (UVIKO 19) kumevuruga mifumo ya maisha na kuzalisha changamoto nyingi sio katika mifumo ya afya pekee, bali pia maisha kwa ujumla,” alieleza Amina.
Akieleza mafanikio yaliyopatikana Zanzibar kupitia umoja huo, Ahmed Rashid, kutoka Shirika la Kuhudumia Watoto Duniani (UNICEF), ni pmoja na kufanyika kwa utafiti wa hifadhi ya mtoto mwaka 2009 uliowezesha kutambua athari zinazowapata watoto.
Katika
kilelel hicho, pamoja na shughuli nyengine, Dk. Mwinyi anatarajiwa kukabidhi
zawadi kwa washindi wa andiko la mradi wa ujasiriamali katika maswala ya uchumi
wa buluu ambapo jana kulifanyika shughuli za usafi wa mazingira katika fukwe za
malindi na upandaji miti kwenye kingo za Mtoupepo.
Comments
Post a Comment