Wanahabari watakiwa kuzingatia usalama wao wakiwa kazini



NA KHAMISUU ABDALLAH

MJUMBE wa Bodi ya Wakurugenzi wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Mussa Yussuf, amewataka waandishi wa habari kujiunga na jumuiya za waandishi ili kuzungumzia changamoto zinazowahusu na kuzipatia ufumbuzi.

Mussa ambae pia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari mkoa wa Dodoma alitoa kauli hiyo wakati akifunga mafunzo ya ulinzi na usalama kwa wanahabari yaliyofanyika jjini Dodoma.

Alisema ikiwa wanabari watajiunga na jumuiya hizo, changamoto nyingi zinazowakabili wandishi wa habari na taaluma ya uandishi wa habari zitapatiwa ufumbuzi na kuleta mabadiliko katika utekelezaji wa majukumu yao.

Hata hivyo alikemea tabia ya makundi ndani ya jumuiya hizo na kueleza kuwa ni adui anaeharibu jumuiya zao kutofikia malengo waliyojiwekea.

“Tunapokutana lazima tuzungumze madhaifu yetu kwani moja ya vitu vinavyoharibu jumuiya nyingi za wanahabari ni makundi na yamejigawa zaidi kimaslahi ni wakati wa kuyasema haya ili kuzijenga jumuiya zetu,” alibainisha Mwenyekiti Yussuf.

alisema ikiwa wanachama na viongozi watasimama imara na kuvunja makundi waliyoyaweka ndani ya jumuiya zao na kuambizana ukweli basi watazijenga jumuiya zao kuwa imara wakati wote.    

Akizungumzia suala la ulinzi na usalama wa waandishi wa habari, alisema ni jambo la msingi kwa wanahabari kuweka kipaumbele katika usalama wao binafsi ili kuwa anakuwa salama wakati wote.

“Usalama wa wanahabari ukitetereka inayopata hasara zaidi ni jamii ambayo inamtegemea katika kupata habari hasa za maendeleo ya taifa lao,” alieleza.

Awali akitoa maelezo ya mafunzo hayo, Afisa Miradi anaeshughulikia mafunzo na machapisho wa UTPC, Victor Maleko aliwasisitiza wanahabari waliopata mafunzo hayo kueneza utaalamu huo kwa wenzao ili wengi wanufaike.

Aidha aliwashauri kutambua mipaka ya kazi zao kwa kufuata misingi ya kazi yao sambamba na kutumia mbinu mbali mbali wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Jumla ya wanahabari 100 kutoka mikoa mbali mbali ya Tanzania bara na Zanzibar wanatarajiwa kupatiwa mafunzo ya ulinzi na usalama kupitia mradi huo wa miaka miwili unaotekelezwa kwa pamoja kati ya UTPC na shirika la International Media Sapport (IMS).

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango