Puma yawatunza vinara kampeni usalama barabarani

  • Ni wanafunzi walioshiriki shindano la michoro

NA MWANDISHI WETU

WADAU wa usalama barabarani nchini limaetakiwa kuchukua hatua kwa madereva wanaofanya matumizi yasiyo sahihi ya barabara ili kuona kiwango cha ajali barabarani kinapungua.

Meya wa Jiji la Zanzibar, Mahmoud Mohammed Mussa, aliyasema hayo alipokua akikabidhi zawadi kwa wanafunzi waliofanya vizuri kwenye zoezi la uchoraji lililoandaliwa kupitia kampeni ya kupunguza ajali za barabarani, hafla iliyofanyika Skuli ya Kiembesamaki ‘A’, Zanzibar.

Alisema ni vyema kudhibiti matumizi yasiyo salama kwa madereva wa vyombo vya usafiri barabarani kwa kuona madereva wote wanafuta sheria na taratibu zilizowekwa.

Mahmoud alisema hatua hiyo lazima iende sambamba na kufanya udhibiti wa vyombo visivyo fuata utaratibu wa matumizi sahihi ya barabara ili kuepusha ajali zisiso za lazima.

Alieleza kuwa kikosi cha Polisi wa Usalama Barabarani kinapaswa kusimamia utekelezaji wa sheria za usalama kikamilifu kwa kuongeze nguvu katika kudhibiti ajali za barabarani.

Hata hivyo alitaka jeshi hilo kufanya zoezi la msako maalumu ili kuona madereva wanaoendesha vyombo hivyo wanakua na leseni zinazotambulika kisharia kwa lengo kuondoa kero za watoto ambao mara nyingi wanatumia barabara wakati wa kwenda na kurudi skuli.

Aliwaomba wafadhili wa mradi huo kuendelea kutoa elimu ya kuhamasisha umma juu ya usalama barabarani kwa watumiaji wa barabara na katika skuli za msingi na sekondari maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba ili kuona wanafunzi wote wanakua salama sambamba na kufikia lengo husika la maradi.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Zanzibar Fatma Rajab alipongeza wadau wa mradi huo uliokusudia kuondoa hofu jamii ikiwemo walimu na wazazi juu ya sula zima la ajili kwa wanafunzi.

Katibu huyo aliwapongeza walimu wa skuli mbali mbali kwa kuibua vipaji vya wanafunzi, hivyo alisema kupitia wizara hiyo inawajibu wa kuendeleza vipaji vya wanafunzi na kuona wanapata mafanikio na kunyanyua vipaji vyao.  

Kwa upande wake, Meneja wa Mauzo wa rejareja wa Puma Energy Tanzania, Venessy Chilambo, alisema suala la usalama barabarani limepewa kipaumbele na kuwekewa mkazo zaidi kutokana na kuonekana limeathiri zaidi wanafunzi ambao ndio viongozi wa baadae.

Alisema mafunzo hayo yamesaidia kupunguza ajali kwa wanafunzi ambao ndio tegeo la taifa hili kwa kupata wanafunzi salama wenye uelewa wa kujikikinga na kujiepusha na ajali zisizo za lazima kutokana na kupewa elimu hiyo mapema wakiwa maskulini.

Alieleza kuwa takwimu za shirika la afya ulimwenguni (WHO), zinaonesha zaidi ya watu milioni 1 wanapata ajali kutokana na matukio mbalimbali yanayosababishwa na vyombo vya usafiri barabarani hivyo kila mmoja anapaswa kuchukua hatua za kupunguza tatizo hilo.

Alifahamisha zaidi ya wanafunzi 40,000 wamepatiwa mafunzo hayo kwa upande wa skuli za Zanzibar kutokana na shughuli za kijamii kuongezeka na kuongezeka kiwango cha magari hapa nchini.

Mapema Mkuu wa kituo cha polisi Mazizini, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP), Salum Amir Ngayana, alisema kampeni hiyo inaenda kuimarisha usalama ambapo kwa kiasi kikubwa itapunguza ajali zisizo za lazima kwa watoto.

Alisema mara nyingi uzembe wa madereva wa barabarani ikiwemo suala la kuacha kufuata sheria na alama za barabarani ndi chanzo cha ajali zinazojitokeza, hivyo alitumia fursa hiyo kuwataka madereva wote kufuata sheria bila shuruti ili kumaliza suala la ajali za barabarani.

Nae Meneja wa AMEND Tanzania, Neema Swai, alisema mradi huo umelenga wanafunzi wa skuli za msingi ili kubadilisha tabia za matumizi ya barabara wakiwa na umri mdogo hali ambayo itapunguza tatizo hilo kwa kipindi kinachokuja.

Alisema mafunzo hayo ni chachu ya watoto wa skuli za msingi kujua namna bora ya kujiepusha na kujikinga na ajali zisizo za lazima hivyo aliomba jamii kutoa mashirikano zaidi kufanisha jitihada hizo kama walivyokusudia.

Zoezi la kukabidhi zawadi limefanyika kwa wanafunzi wa skuli za msingi, Bububu, Mtopepo, Kiembesamaki, Dole na Fuoni ambapo mshindi wa kwanza alikuwa Khalid Mohammed Said wa Mtopepo, aliyezawadiwa shilingi 500,000 wakati skuli yake ilipatiwa shilingi Milioni 4 zilizotolewa na Puma Energy Tanzania.


Meya wa Jiji la Zanzibar, Mohamoud Mohamed Mussa(watatu kulia) akikabidhi kikombe kwa mshindi wa Shindano la michoro wa Usalama Barabarani kwa skuli  za Msingi Zanzibar lililondaliwa na Kampuni ya Mafuta ya Puma Tanzania kwa kushirikiana na AMEND Africa, Khalid Mohamed Said anayesoma darasa la sita skuli ya Msingi Mtopepo 'B' Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango