Mtoni
Kidatu wahimizwa kulinda maeneo ya skuli
NA
MWANDISHI WETU
MKUU
wa Wilaya ya Magharibi ‘A’ Suzan Peter Kunambi, amewataka wananchi wa wilaya
hiyo kuhakikisha wanalinda rasilimali ya ardhi ya elimu ili kuona hayavamiwi
kiholela.
Kauli hiyo aliitoa wakati
akizugumza na wananchi wa Mtoni Kidatu alipokuwa akisikiliza changamoto
zinazowakabili walimu wa skuli ya Mtoni Kidato.
Alisema kuna uvamizi mkubwa katika
maeneo ya skuli zilizomo ndani ya wilaya yake kutokana na wananchi kujenga
makaazi ya kudumu.
“Sio skuli hii tu iliyovamiwa,
skuli vinazovamiwa ni nyingi hivyo ni wajibu wa wananchi mliopo karibu na
maeneo ya skuli mnapoanza ujenzi msikae kimpya kwani mipaka ya skuli
inajulikana na kuwasisitiza walimu kuacha kuazima maeneo ya skuli,” alisisitiza.
Alisema ni vyema kuwa walinzi wa
maeneo hayo kwani bado yana shughuli kubwa kwani bado miundombinu ya elimu
inahitajika kujengwa ya kisasa.
Aidha alisema maeneo mengi
yanavamiwa na pale serikali inapotaka kujenga majengo ya horofa ya skuli inakuwa
na changamoto kubwa ya kukosa maeneo kutokana na maeneo mengi kuvamiwa.
“Haya ndio yanayotukuta sasa hivi,
wizara imepanga kutujengea skuli ya ghorofa katika eneo la Mtopepo hatuna eneo
kwani eneo lote limevamiwa sasa niwaombe eneo hili ambalo bado lipo kidogo basi
ni sote tulilinde,” alisisitiza Kunambi.
Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo, Haidar
Yahya Issa, alisema skuli yao inakabiliwa na changamoto kubwa wa uvamizi wa
maeneo yao kwa maakazi ya nyumba hali
ambayo inatokana na kukosa kwa hatimiliki ya eneo lao.
Nae Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Amal, Ali Khamis Juma,
alisema ni kweli maeneo mengi ya skuli yamekuwa yakivamiwa kwa maakazi hivyo
aliziomba ofisi za wilaya, shehia na kamati za skuli kuhakikisha wanasaidia
kutovamiwa kwa maeneo ya skuli.
Aidha Katibu Ali alisema serikali na
wafadhili wengine zinajitahidi kuongeza miundombinu nzuri katika skuli zake
lakini wapo watu wachache wanaona mambo hayo sio muhimu hivyo ni vyema
kudhibitiwa watu hao kwa nguvu zote.
Mwalishi wa Jimbo la Mwera, Mihayo
Juma N’gunga ni alikiri baadhi ya wananchi kujimilikisha baadhi ya maeneo ya
skuli kwa ujenzi wa nyumba za makaazi hasa katika skuli zote zilizokuwepo ndani
ya jimbo hilo.
Aliyataja maeneo hayo alisema ni
pamoja na skuli ya Mtoni Kidatu, Regezamwendo, Kianga, skuli ya Chunga
changamoto ambayo ipo kwa asilimia kubwa katika Mkoa huo.
Aliahidi kuwa kwa kushirikiana na
serikali ya wilaya na mkoa wanategeneza utaratibu maalum kwa watu wote
wanaovamia na kuhakikisha skuli zote zilizokuwepo ndani ya jimbo hilo zinapata
hati za maeneo yao ili kuweza kulinda mipaka yake.
Alisema kuvamiwa kwa maeneo mengi
ya skuli kunatokana na kukosekana kwa hatimiliki jambo ambalo linatakiwa
kufanyiwa kazi kwa nguvu zote.
Alitumia fursa hiyo kuwasisitiza
wananchi kuacha tabia ya kuvamia maeneo ya skuli ili kuweza kusaidia ujenzi
pale serikali inapotaka kuongeza madarasa kwa ajili ya kuhakikisha watoto
wanapata elimu katika maeneo ya karibu.
Comments
Post a Comment