ZPC, CPS Ltd zaazimia kuimarisha ushirikiano

NA MWANDISHI MAALUM

KATIKA kuimarisha mahusiano na ushirikiano kati ya Klabu ya Wandishi wa Habari Zanzibar (ZPC) na wadau wake, viongozi  wa klabu wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti,  Tabia Makame Mohammed (Februari  7, 2022)  wametembelea na kufanya mazungumzo na Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya CPS Ltd Tobias Dietzold.

kampuni ya CPS Ltd inayojenga Mji wa Maendeleo wa Fumba (Fumba Town Development) uliopo Nyamanzi, wilaya ya Magharibi ‘B’, Unguja imekuwa na mahusiano ya karibu ya kikazi na klabu hiyo toka mwaka 2016 ambapo zimekuwa zikishirikiana katika mambo mbali mbali.

Katika  mazungunzo yao, pande mbili hizo zimebadilishana mawazo na kukubaliana kuimarisha mahusiano na kushirikiana katika utekelezaji wa malengo na majukumu ya taasisi hizo hususani kutoa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kuwa na makaazi bora kama ilivyo katika sera na mipango yanserikali.

Aidha Tobias aliipongeza ZPC kwa kuendelea kuwa karibu na kampuni yao na kuahidi kushirikiana na vyombo vya habari vya Zanzibar kuijumisha jamii dhamira ya uwekezaji wanaoufana nchini.

"Tunashukuru siku zote mmekuwa pamoja nasi na kutusaidia kutambulisha mradi wetu ambao upo kwa ajili ya Wazanzibari ili kukabiliana na changamoto ya ufinyu wa ardhi na mahitaji ya makaazi," alieleza Tobias.

Alieleza kutokana na ongezeko la watu, kumekuwa na majitaji makubwa ya makaazi hivyo ipo haja ya nchi kuwa na mikakati ya kuhifadhi aradhi kwa kujenga nyumba imara katika eneo dogo.

Nao viongozi wa klabu hiyo walieleza kufurahishwa kwao na maendeleo ya utekelezaji  wa mradi huo unaohusisha nyumba za chini na ghorofa.

Aidha viongozi hao walipata taarifa mbali mbali zinazohusu utekelezaji wa mradi huo na kuwaomba kutumia vyombo vya habari kutangaza mradi huo.

PICHA

Makamu Mwenyekiti wa ZPC, Tabia Makame Mohammed (kulia) akiongoza kikao kati ya viongozi wa klabu na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya CPS Limited, Tobias Dietzold, kilichofanyika katika ofisi za kampuni hiyo Nyamanzi.

Wajumbe wa Kamati Tendaji ya ZPC wakiongozwa na Afisa Masoko na Biashara, Paul Wangoma (kulia) walipotembelea maeneo yanayoendelea na ujenzi katika Mji wa Maendeleo wa Fumba (FTD) walipofanya ziara na mazungumzo na uongozi wa kampuni ya CPS Ltd.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango