Watendaji OMKR wakiwa kuongeza ubunifu


NA RAYA HAMAD, OMKR

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Dkt. Saada Mkuya Salum (katikati), amewataka Watendaji wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Zanzibar kuendelea kuwa wabunifu ili kwenda sambamba na maono ya Serikali ya awamu ya nane ya kutimiza matarajio ya kuwatumikia vyema wananchi.

Dkt. Mkuya ameyasema hayo wakati wa makabidhiano ya ofisi baina yake na Waziri mpya wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Harous Said Suleiman kufuatia mabadiliko ya baraza la Mapinduzi  yaliyofanywa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Mwinyi hivi karibuni.

Amesema kwamba wananchi wanamatarajio makubwa ya Serikali ya awamu ya nane katika utekelezaji wa sera na mipango mbali mbali ya maendeleo na kwamba ni vyema wafanyakazi kujitahidi kwenda sambamba na matarajio hayo.

Hata hivyo, Dkt Saada amewakumbusha watendaji hao pia kujitahidi kuenda na muda kwa kuzingatia  wakati katika utekelezaji wa shughuli za kazi mbali mbali ili kumsaidia waziri Harusi kutimiza vyema majukumu yake.

Amehimiza wafanyakazi hao kumpa mashirikiano Waziri Harusi kama walivyompa yeye ili aweze kutumiza majukumu yake kwa wepesi na kuweza kupata mafanikio katika sekta zote mtambuka anazoziongoza ndani ya wizara hiyo.

Naye waziri mpya wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Harusi Said Suleiman, amewaomba wafanyakazi hao kumpa mashirikiano katika kufanikisha utekelezaji wa shughuli za Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais na ujenzi wa nchi kwa jumla.

Amewakumbusha watendaji hao umuhimu wa kuendelea kufanyakazi kwa mashirikiano na kuheshimu sheria na taratibu za kazi kama msingi wa mafanikio   kazini.

Aidha Harusi amezitaka taasisi zote za ndani kuhakikisha kwamba zinatayarisha na kutekeleza mpango mkakati katika utekelezaji wa malengo ya taasizi husika.

Naye Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Dk. Omar Dadi Shajak, amemshukuru waziri aliyeondoka Mhe. Dkt Saada Mkuya kwa usimamizi bora kwa kipindi chote alichokuwepo kwa kutumia umahiri na maono mapana katika kusimamia sekta zilizopo ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais.

Dkt. Shajak amesema kwamba katika kipindi kifupi alichoiingoza Ofisi hiyo usimamizi wake umeleta ufanisi kwa kutekeleza mambo mengi likiwemo suala la mabadiliko ya sheria ya kupambana na dawa za kulevya Zanzibar. 

Makabidhiano hayo yamefanyika kwenye ukumbi wa mkutano wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Migombani, Zanzibar.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango