Ujerumani kusaidia utafiti wa maji Z'bar

ZANZIBAR

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) na Serikali ya Shirikisho la Ujerumani zimetiliana saini mkataba wa ruzuku ya utafiti na upembuzi yakinifu katika sekta ya maji unaolenga kujua ubora na wingi wa maji yanayopatikana Zanzibar.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Dk. Juma Malik Akil (kulia), akisaini makubaliano ya ruruku kwenye utafiti na upewa majihayo pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Dk. Salha Kassim (kushoto) na Naibu Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Kibenki la Ujerumani, Andrea Hoeltke (katikati).

Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Johannes Sperrfechter ameishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa juhudi na ushirikiano wao ambao unalenga kujenga maisha bora ya Wazanzibari.

Alisema hatua hiyo ni mwendelezo wa ushirikiano mpya wa kimaendeleo kati ya Ujerumani na Zanzibar uliozinduliwa mwezi Januari 2022 kwa pamoja na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi na Balozi wa Ujerumani.

Katika uzinduzi huo, ujerumani iliahidi kuisaidia Zanzibar katika maeneo mbali mbali yakiwemo ya uimarishaji wa sekta zinazohusiana na maisha ya watu.

Balozi Johannes alisema mchakato wa utafiti na upembuzi yakinifu umeshaanza na masharti ya mkataba yanakaribia kukamilika ambapo mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) na wadau wengine wa maendeleo  watahakikisha wanaongeza ufanisi.

“Matarajio yetu kupitia mpango huu ni kupata maarifa muhimu ya usimamizi endelevu wa rasilimali za maji Zanzibar kwa kufanya utafiti wa maji yaliyopo chini ya ardhi,” amesema balozi Johannes.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Dk. Saada Mkuya Salum alisema Zanzibar pamoja na kuwa ni nchi ya visiwa lakini imekuwa ikibabiliwa na changamoto ya maji kwa wananchi wake.

Alisema kutokana na hali hiyo ndipo Serikali ya Ujerumani imekubali kuwapatia msaada wa Euro milioni 6.6 sawa na shilingi Bilioni 1.7 za Tanzania zitakazotumika kwa utafiti huo pamoja na mambo mengine yanayolenga kujua ukubwa wa tatizo hilo nchini.

Aliipongeza serikali ya Ujerumani kwa kuamua kusaidia mradi huo ambao Zanzibar inakwenda kutekeleza kwa vitendo mpango wa maendeleo wa miaka mitatu na mpango mkuu wa 2025 unaolenga kuimarisha upatikanaji wa maji safi na salama Zanzibar.

“Kwa upande wetu Serikali tutausimamia utekelezaji wa mradi huu utakaotekelezwa maeneo mbali mbali ya na kuhakikisha tunafikia malengo tuliyojiwekea,” alisema.

Hafla ya utiaji wa saini ilifanyika katika ofisi za Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Kinazini Zanzibar na kushuhudiwa na viongozi hao wa serikali ya Zanzibar na Ubalozi wa Ujerumani nchini.  


Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango