Wanufaika TASAF wataja mafanikio

NWANDISHI WETU, PEMBA

WANUFAIKA wa mpango wa kunusuru kaya masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF), kisiwani Pemba wamesema miradi waliyoibua imewakomboa kiuchumi na kumudu gharama za kusomesha watoto wao skuli.

Walisema miradi mingi waliyoianzisha kutokana na ruzuku wanazopokea kupitia mpango huo, imewatoa kutoka katika dimbwi la umasikini na sasa wana uhakika wa kupata kipato cha kujikimu kimaisha.

Mmoja ya wanufaika hao, Bahati Vuai Haji wa kijiji cha Kwareni Vitongoji, mkoa wa Kaskazini Pemba alieazisha biashara ya mgahawa wa chakula, alisema kuwa kabla ya kuwezeshwa na TASAF hali yake kiuchumi ilikuwa ngumu.

Alisema baada ya kupitia ruzuku hiyo aliweka akiba na kuanzisha biashara ya bagia na kujiunga katika vikundi vya kuweka na kukopa hatimaye kuazisha mgahawa wa chakula (Mamantilie) ambapo kwa sasa ndio kazi inayoendesha familia yake ya watoto watano.

 “Nashukuru hivi sasa napata fedha familia yangu inapata huduma ya chakula na nyengine maana kabla ya kupatiwa ruzuku nilikuwa Napata shida kuwahudumia watoto wangu kwa sababu baba yao hana msaada wowote,” alisema.

Bahati alisema biashara hiyo imemuwezesha kununua kiwanja, kusomesha watoto wake na kulisha familia angalau kwa milo miwili kuliko ilivyokua kabla.

Hata hivyo mnufaika huyo alisema kuwa bado mtaji wake ni mdogo hivyo anahitaji fedha kwa ajili ya kuboresha biashara zake ili huduma anayoitoa kuwa na ubora.

Mnufaika mwengine Saumu Amour Muhammed, mkaazi wa kijiji hicho, alisema baada ya kupata ruzuku ya shilingi 84,0000 kutoka TASAF alianza kufanya biashara ndogo ndogo na kujiunga na vikundi vya kuweka na kukopa na faida aliyoipata akaanza na kilimo cha mboga na matunda.

Alisema kilimo hicho kimekuwa ni tegemezi kwa familia yake lakini changamoto kubwa aliyonayo ni uhaba wa maji kwa ajili ya umwagiliaji wa kilimo chake na kuiomba Serikali kuendelea kuwapatia elimu na mitihaji ili kukuza biashara zao na kutoa ajira kwa watu wengine.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango