Msando awataka waandishi kutete haki za binadamu
NA MADINA ISSA
MKUU wa wilaya ya Morogoro, Albert Msando, amewataka wanahabari nchini kuendelea kufanya kazi kwa bidii na weledi zikiwemo za utetezi wa haki za binadamu ili kuongeza tija katika kutoa habari kwa wananchi.Aliyasema hayo alipokuwa akifungua
mafunzo ya siku mbili kwa wanahabari yanayohusu namna bora ya kutoa habari yaliyoratibiwa
na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), yanayofanyika mkoani
Morogoro.
“Mwandishi wa habari mzuri ni yule
anayetoa taarifa zinazozingatia ukweli, usahihi na kutopendelea ili jamii
inufaike na wenye mamlaka wachukue hatua zinazostahiki,” alieleza Msando.
Aidha aliwataka wanahabari
kujitahidi kuwa watetezi wa haki za binadamu bila ya ushabiki au kuegemea
upande mmoja ili kuepukana na changamoto mbali mbali zinazoweza kuwatokea.
“Tujitahidini sana kuishi katika
utetetezi wa haki za binaadamu na tusimameni katika ukweli na haki na wala
tusiwe chanzo cha machafuko badala yake tuache habari ifike kama ilivyo ili
wananchi wamue,” alieleza.
Alisema kuwa serikali ya awamu ya
sita haina nia ya kuwanyima wanahabari uhuru wao wa kutoa habari na hakuna
sababu ya kuishi kwa woga na kuwahimiza kuendelea kufanya kazi kwa mujibu wa
misingi ya sheria na miongozo ya kihabari iliyopo.
Nae Jaji Mstaafu Robert Makaramba,
alikiwasilisha mada ya namna ya kuandika na kuripoti habari za mahakamani,
alisema kuwa ni vyema wakaepuka kutoa taarifa ambazo hazijatolewa mahakamani
ili kuepusha sintofahamu kwenye jamii.
Jaji Makambara aliwataka waandishi
wa habari kuzingatia taratibu na kanuni zilizopo huku akikiri kuwepo kwa baadhi
ya sheria kandamizi ambazo, alishauri haja ya kufanyiwa marekebisho.
Awali akizungumza Wakili kutoka
THRDC, Leopold Mosha, alisema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo waandishi
wa habari juu ya namna ya kuandika na kuripoti taarifa zinazohusiana na haki za
binadamu kutoka mikoa mbali mbali nchini.
Alisema THDRC imebaini kuwepo kwa
changamoto mbali mbali katika kuripoti masuala yanayoendana na kisheria jinsi
ya kutoa taarifa za kesi mahakamani na maamuzi ya kimahakama.
“Tulibaini kwamba taarifa nyingi zilikuwa
zinatolewa na mapungufu ikiwemo kiufundi na zimekuwa zinaleta mkakasi katika jamii,”
alieleza Wakili Mosha.
Hivyo, alisema kupatiwa mafunzo
hayo, yatawawezesha wanahabari kujua vigezo na maeneo ya kisheria wanayopaswa
kuzifuata wakati wanaporipoti kesi mbalimbali ambapo nchi ipo na sheria.
Kwa upande wake Afisa Uchechemuzi wa
THRDC, Nuru Maro, akiwasilisha mada ya umuhimu wa waandishi wa habari katika kufanya
uchechemuzi wa masuala mbali mbali alisema ni vyema waandishi kufahamu chanzo,
ushahidi, kujua watu wengine wanavyofanya kazi hilo eneo husika.
Aidha alisema kuwa waandishi wa
habari ni daraja la kuwaunganisha wannachi wote hivyo watumie kalamu zao ili
kuona hali inaendelea kuwa nzuri na kufikisha ujumbe kwa jamii ukiwa na hali
halisi na ukweli ndani yake.
Baadhi ya wanahabari wanaoshiriki
mafunzo hayo, waliahidi kufanya kazi kwa mujibu wa sheria zilizopo sambamba na
kuibua kitu mambo yatakayoleta mabadiliko katika utendaji na jamii kwa ujumla.
Comments
Post a Comment