JMKF, PIT zawanoa wasichana kufikia ndoto zao
DAR ES SALAM
Mafunzo
hayo yaliyopewa jina la ‘Wasichana Washika Hatamu’ yaliandaliwa na taasisi za Jakaya
Mrisho Kikwete Foundation (JMKF) kwa kushirikiana na shirika la Plan
International Tanzania (PIT), yalifanyika kwa siku mbili katika hoteli ya
Regency Park jijini Dar es salaam.
Akizungumza
wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa JMKF, Vanessa
Anyoti, alieleza kwamba imekuwa jukwaa muhimu katika kutambua haki za
msichana na changamoto kubwa anazopambana nazo duniani.
“Tanzania inaungana na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa katika kukuza ufahamu wa jamii juu ya masuala yanayowakabili wasichana na kuwapatia fursa ya kupaza sauti zao,” alisema mkurugenzi huyo.
Aliongeza
kuwa duniani kote wasichana wanaendelea kukabiliana na changamoto za uongozi,
elimu, masuala ya afya ya akili na ukatili wa kijinsia hivyo kuna haja ya
kuwajengea uwezo ili wawe mawakala wakuu wa mabadiliko katika jamii zao.
Mafunzo
hayo ambayo ni sehemu ya shughuli za kuelekea kilele cha siku ya kimataifa ya
mtoto wa kike inayoadhimishwa kila ifikapo Oktoba 11 ya kila mwaka
yanalenga kuwawezesha wasichana na kukuza sauti zao.
Aliongeza
kuwa kwa kushirikiana na wadau wengine, taasisi yake itaongeza uwezo wa vijana
wasichana wa kujiamini, kutambua afya ya akili, kukuza
ustawi wao hususani katika masuala ya lishe na ukakamavu.
Aliyataja
maeneo mengine kuwa ni ya kutambua haki za mtoto wa kike pamoja na ufahamu wa
sheria za nchi juu ya maswala yanayowahusu chini ya kauli mbiu ya maadhimisho
hayo Duniani inayosema; ‘Wakati wetu ni sasa — haki zetu, mustakabali
wetu’.
Comments
Post a Comment