Mbunge ataka vijana kutambua nafasi zao kwenye maendeleo

NA SAIDA ISSA, DODOMA

MBUNGE wa Viti Maalum, Nusrat Hanje, amesema katika kuhakikisha mchango wa vijana unaonekana kwenye maendeleo ya taifa vijana wanatakiwa kutambua nafasi yao na nguvu ya ushawishi waliyonayo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa ‘Vijana Makini’, jijini Dodoma alisema serikali ina wajibu wa kutengeneza mbinu wezeshi kwa kuwafanya vijana wanajibika kwa kua kundi hilo lina idadi kubwa ya watu nchini.

"Vijana ni sehemu kubwa katika nchi yetu, nikiwa Mbunge kijana naishauri serikali yetu kuwatengenezea mbinu wezeshi vijana hawa ambao ndio taifa la kesho,” alieleza Mbunge huyo.

Aliongeza kuwa iwapo serikali itaweka misingi imara na thabiti kwa vijana wa leo hapo baadae hakutakuwa na changamoto katika taifa kwani watakua imewekeza katika eneo salama.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Msaidizi, Uratibu na Uwezeshaji kiuchumi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu, Eliakim Mtawa alisema mara nyingi vijana ndio wenye tatizo kwani wanapopata fedha huzitumia kwa malengo yasiyokusudiwa.

“Serikali inatoa hela kwenu lakini nyinyi ni shida pia hamshiriki katika vikao vya chini kujadili mambo yenu bali mnakuja kwenye ngazi za juu na kudai wakati kule chini hampo nani atayasemea mambo yenu,” alihoji Mtawa.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Dira ya Vijana Tanzania (TYVA), Yusuph Bwango, alisema lengo la mradi huo ni kuhakikisha vijana wanakuwa na ushiriki madhubuti katika ushwawishi na utetezi  wa masuala yanayowahusu na kwenye mchakato wa bajeti ya serikali.

Alisema mradi huo unalenga kujumuisha taasisi za vijana mbali mbali za vijana zitakazounda mwamvuli utakao wawakilisha kwenye jukwaa la utetezi wa bajeti ya vijana.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango