SMZ yaweka sawa taarifa kuhusu Mkurugenzi ZIPA
NA ABOUD MAHMOUD
SERIKALI imekanusha taarifa zilizozagaa mitandaoni zinazomuhusu Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Uwekezaji na Ukuzaji Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA), Shariff Ali Shariff, kuhusishwa na tuhuma za ujasusi.
Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mudrik Ramadhan Soraga, katika Ofisi za Mamlaka hiyo, huko Maruhubi wilaya ya Mjini Unguja, alisema tuhuma hazina ukweli wowote na zimelenga kumchafulia jina mtendaji huyo mzalendo kwa nchi yake.
Alieleza kwamba
tuhuma zinazohusiana na mtendaji huyo kuwa na hati mbili za kusafiria
zinaonekana kuwepo kwa watendaji wasio waaminifu wenye kuchezea mifumo ya nyaraka
za Serikali.
"Kitendo
kilichofanywa cha kumchafua mtendaji huyu sio kizuri kwani ni cha uongo hivyo
hatutokua tayari kuona watendaji wanaharibiwa majina na naahidi uchunguzi kwa
hatua zaidi,"alisema.
Aidha Soraga
aliwaomba wandishi wa habari kuacha kuyatumia vibaya majukwaa yao na kuendelea
kufanya kazi kwa kuzingatia miko na maadili.
Nae Shariff aliitaka jamii pamoja na wana
habari kufanya uchunguzi kabla ya kusambaza taarifa ili kujua ukweli na sio
kutoa shutuma zisizokua na uhakika.
Tuhuma
zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii zinamuhusisha Mkurugenzi huyo na
mdogo wake ambae ni pacha anaeishi Jamuhuri ya watu wa Czech.
Ndugu yake huyo
alikuja nchini na familia yake ambapo alipoondoka na kuonekana hati yake ya
kusafiria ya nchi anayoishi zikasambazwa taarifa kuwa mtendaji huyo ana hati za
uraia wa nchi mbili tofauti.
Comments
Post a Comment