Waliojenga viwanja vya serikali kukiona
NA MWANDISHI WETU
WAZIRI wa Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, Rahma Kassim Ali, amewataka watu waliovamia eneo la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar liliopo Tunguu, mkoa wa Kusini Unguja na kujenga kinyume cha sheria, kusimamisha ujenzi huo hadi serikali itakapotoa maamuzi.
Waziri
Rahma alitoa agizo hilo hivi karibuni alipofanya ziara ya kutembelea eneo akiambatana
na baadhi ya watendaji wa wizara na ofisi ya mkuu wa mkoa kusini Unguja akiwemo
mkuu wa mkoa huo, hadid Rashid hadid.
Ziara
hizo nio sehemu ya utaratibu aliojiwekea wa kutembelea maeneo ya serikali ambayo
baadhi ya wananchi huvamia na kujenga bila ya kua na kibali rasmi cha ujenzi
hali inayopelekea kurudisha nyuma. jitihada za kuleta maendeleo nchini.
“Kuna
baadhi ya wananchi wanapoona maeneo ya wazi huyavamia na kuanza ujenzi bila ya
kutambua kuwa maeneo hayo ni ya serikali hivyo wale wote waliovamia eneo hili,
kuanzia leo wasitishe mara moja ujenzi huo na atakaekwenda kinyume na agizo
hilo hatua za kisheri zitachukuliwadh yake,” alieleza Waziri huyo.
Aidha
Waziri huyo alitoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanafuata sheria na taratibu zilizowekwa
wanapohitaji kufanya ujenzi kwa kufika katika taasisi zinazohusika kupata
vibali na klupimiwa maeneo hayo ili kuepusha migogoro ya ardhi inayojitokeza
nchini.
"Ili
kuepusha migogoro ya ardhi nchini ambayo mengine husababishwa na uvamizi wa maeneo
kinyume na utaratibu, niwaombe wananchi wanapotaka kufanya ujenzi kufika katika
taasisi husika kwa lengo la kupatiwa utaratibu mzuri wa kisheria," alisema
Waziri Rahma.
Kwa
upande wake Mkuu wa mkoa Kusini Unguja, Rashid Hadid Rashid, alisema kwa
kushirikiana na Ofisi za Mkuu wa Wilaya watahakiksha wanayasimamia
ipasavyo maeneo yote waliyovamia na wananchi ili wasiendelee na ujenzi huo kwa
maslahi ya nchi na watu wake.
"Kuna
uvamizi mkubwa ambao umefanywa na baadhi ya wananchi ndani ya eneo hili jambo
ambalo linasikitisha hivyo nitahakikisha ninalisimamia kwa kuwaita wahusika
waliofanya ujenzi na kuwataka kuchukua hatua za kuhama mara moja," alisema
Hadid.
Nae
Mkurugenzi Upimaji na Ramani kutoka Kamisheni ya ardhi, Juma Ameir, alieleza
kusikitishwa kwake na tabia ya baadhi ya wananchi hao kuvamia hadi kiwanja cha
mpira ambacho kilishashapimwa na kukabidhiwa taasisi husika.
Ziara
ya Waziri Rahma katika maelneo hayo ililenga kuangalia hali halisi ya uvamizi
katika maeneo ya ambayo wananchi huvamia kinyume na sheria kwa ajili ya kuyatafutia
ufumbuzi.
Comments
Post a Comment