Senyamule awaita watanzania kupokea matokeo ya sensa

NA SAIDA ISSA, DODOMA

MKUU wa Mkoa wa Dodoma,  Rosemary Senyamule ametoa wito kwa wakazi wa Dodoma kuhudhuria  kwa wingi katika viwanja vya Jamhuri kushuhudia uzinduzi wa matokeo ya  mwanzo ya sensa  ya watu na makazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma Senyamule wakati wa hafla ya uwekaji jiwe la msingi ujenzi wa uwanja wa ndege wa kimataifa wa Msalato Oktoba 30, mwaka huu amesema  ni vyema wana-Dodoma na Watanzania  kwa ujumla kushiriki katika shughuli hiyo ya kihistoria kufuatia sensa inayofanyika kila  baada ya miaka 10.

"Ni siku ya kipekee na hapa tuna siku moja kufika siku ya kutangaziwa matokeo na Mheshimiwa Rais  wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, nitoe shime wana Dodoma mje  kwa wingi kuanzia saa 12 asubuhi hapa kwenye viwanja  vya Jamhuri,” amueleza Mkuu huyo wa mkoa.

"Leo (31 Oktoba) kuanzia saa 6 usiku tutakuwa na shamra shamra ya kupiga fataki zikiashiria kuwa Dodoma tupo tayari kuletewa matokeo ya  sensa ya watu na makazi  hivyo tujitokeze Kwa wingi wana Dodoma" amesema Senyamule

Hata hivyo uzinduzi wa matokeo hayo yamebebwa na kauli mbiu isemayo  "Matokeo ya sensa ya sita  2022, Mipango jumuishi kwa maendeleo endelevu".

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango