SMZ yajidhatiti kusimamia haki, ulinzi wa watoto

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imesema imejipanga kuimarisha ulinzi na kusimamia upatikanaji wa haki za watoto  katika ngazi ya jamii. 

WAZIRI wa Maendeleo, Jinsia, Wazee, Wanawake na Watoto, Riziki Pembe Juma (pichani), alieleza hayo alipozungumza na mwandishi wa habari hizi wakati wa sherehe  maadhimisho ya miaka 77 ya Umoja wa Mataifa (UN) yaliyofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idriss Abdulwakil, Unguja. 

Amesema hatua hiyo itasaidia kulinda haki, fursa na kuimarisha ustawi na maendeleo hasa katika upatikanaji wa haki za watoto pamoja na kupinga vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto. 

Amesema mikakati huo  utakuwa pamoja na kuwajengea uwezo wa kisheria   wanawake  ili waweze  kulinda na kusimamia haki na  mambo mengine ya msingi ya nayo stahiki kupatiwa watoto. 

Mbali na hilo amesema  Wizara hiyo itafanya kazi kwa karibu na Umoja wa Mataifa  kwa kuhimiza na kushajihisha  wanawake kushiriki katika mchakato wa uchaguzi ili kushika nafasi ya uongozi katika siasa. 

“Miongoni mwa mambo yatakayopewa kupaumbele ni   pamoja na kuongeza nguvu katika kubadilisha mtazamo ya kijamii kisasa na kiuchumi kwa wanawake ili waweze kutumia fursa za maendeleo nchini,” amesema Waziri Pembe. 

Katibu ya Jumuiya ya Kusimamia Haki na Malezi ya Watoto,  Abdulkadir  Nassor,  amesema  ulinzi wa watoto unahitaji nguvu za pamoja  baina ya  serikali na wananchi kwa jumla. 

Amesema serikali imefanya juhudi za kuweka sheria na miongozo ya Kusimamia na kupatikana haki za watoto jambo muhimu ni mashirikiano na uwazi ndani ya jamii na watendaji. 

Nae mkaazi wa Gongoni, Fatma Abeid, amesema moja ya changamoto zinazokwamisha upatikanaji wa haki na ulinzi wa watoto ni ukiukwaji wa maadili na silka za Mzanzibari.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango