TIB yaanika sababu za kuweka riba nafuu mikopo ya kilimo

NA MWANDISHI WETU, MWANZA        

BENKI ya Maendeleo Tanzania (TIB) imepongezwa kwa kutoza riba nafuu kwa wakulima na wawekezaji wanaojishughuisha na za uzalishaji, usindikaji mazao na masoko hasa kwa wakopaji wanaojihusisha na shughuli za uzalishaji na usindikaji wa mazao ya kilimo hapa nchini.  

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Hamad Chande (pichani kushoto), wakati alipotembelea banda la benki ya TIB, kwenye maonesho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yaliyokua yakifanyika katika viwanja vya Rock City Mall, jijini Mwanza. 

Chande alionesha kufurahishwa na huduma za mikopo inayotolewa na benki hiyo kupitia dirisha la kilimo linalowalenga wakulima na wawekezaji wenye miradi ya kilimo na ufugaji. 

Akiwa bada la benki hiyo, Chande alijulishwa kuwa riba inayotozwa kupitia kwa mikopo hiyo ni asilimia tano kwa mwaka kwa wakopaji wa moja kwa moja toka benki na asilimia 4 kwa upande wa taasisi zinazokopa kwa ajili ya kukopesha ambapo hutatakiwa kukopesha kwa asilimia isiyozidi asilimia nane kwa wateja wao. 

Alisema serikali inafarijika kuona TIB inaendelea kuwahudumia wakulima wadogo wadog, wa kati na wakubwa wanaoendesha kilimo cha kibiashara kupitia makampuni ili kuongeza thamani shughuli za kilimo hapa nchini. 

Kwa mujibu wa Afisa Biashara Mwandimizi wa Benki ya Maendeleo (TIB), John Mboje, TIB imekua ikitoa mikopo kupitia Dirisha la Kilimo ambayo kipindi cha marejesho ni kati ya miezi sita hadi miaka 15 kwa kutegemea aina ya mradi wa kilimo pamoja na makadirio ya hesabu

Mboje aliongeza kuwa mikopo hiyo huwa na kipindi cha rehema kinachotolewa kulingana na kipindi cha kukomaa kwa mazao husika pamoja na makadirio ya mtiririko wa fedha ambapo kipindi cha juu cha rehema ni miaka 3 kwa mazao ya muda mrefu na mwaka mmoja kwa mazao ya muda mfupi.  

“Benki ya Maendeleo TIB ni taasisi ya serikali iliyoanzishwa kwa malengo ya kuwezesha upatikanaji wa mitaji ya muda mrefu na wa kati kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi hapa nchini,” alieleza Mboje. 

Benki ya Maendeleo TIB ilishiriki maonesho hayo ya Wiki ya Huduma za Fedha yenye kauli mbiu ‘Elimu ya fedha kwa maendeleo ya watu’ ili kutoa ya kuujulisha umma kuhusu huduma na bidhaa zinazotolewa na benki hiyo. 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango