JUWAZA kuhamasisha upatikanaji haki za wazee
NA MWANDISHI WETU
JUMUIYA ya Wastasfu na Wazee Zanzibar (JUWAZA) imesema itaendelea kuhamasisha upatikanaji wa stahiki za wazee zikiwemo za kiafya ili kupata haki zao na afya zao zinaimarika.
Akitoa taarifa kwa
waandishi wa habari ofisini kwake Migombani, Katibu wa jumuiya hiyo, Salama
Kondo Ahmed, alisema jumuiya imekuwa ikitekeleza kazi zake kwa mashirikiano na serikali
pamoja na taasisi binafsi katika kuhakikisha inafikia malengo yake.
Alisema kuwa idadi
ya watu wenye umri wa miaka 80 na kuendela inakadiriwa kukua kwa mara tatu
zaidi baina ya mwaka 2022 na 2050 na kufikia milioni 426 ulimwenguni hivyo nchi
zinahitaji kujiandaa na kuandaa mazingira ya kukidhi mahitaji ya wazee.
Kondo alisema, JUWAZA
ina mikakati mbali mbali ya kuimarisha ustawi wa wazee na wastaafu itakayotekelezwa
kwa ushirikiano na serikali na taasisi binafsi
“Miongoni mwa mambo
ambayo tumeweza kuyasimamia ni pamoja na kufanya utetezi na kupelekea kuuanzishwa
kwa mpango wa pensheni jamii kwa wazee wote toka mwaka 2008 mpango ulioanza
kutekelezwa 2016,” alisema Kondo.
Alieleza kuwa na mpango huo ulioanza
kutekelezwa mwezi Aprili, 2016 kwa wazee wenye umri wa kuanzia miaka 70 kupokea
shilingi 20,000 kila mwenzi zoezi ambalo linaendelea hadi hivi sasa.
Alitaja mafanikio
mengine ya jumuiya hiyo kuwa ni pamoja na kuundwa kwa mabaraza 342 ya wazee katika
ngazi ya shehia Unguja na Pemba.
Hata hivyo, alisema
kuwa wamefanya ushawishi kuhusu kuanzishwa kwa sheria ya wazee namba 2 ya mwaka
2020 kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambayo
iliwekwa saini mwezi Aprili 2020 na kuanza kutumika.
Kondo alisema kufuatia
ongeeko kubwa la maradhi yasiyoambukiza miaka ya hivi karibuni kumekuwa na
wadau hususani asasi za kiraia zimekuwa zikitoa huduma za maradhi hayo katika
jamii.
“Pamoja na wingi wa
wadau hawa lakini kumekosekana mashirikianao baina yao na hivyo mafanikio
yanapatikana hayafikii kile kiwango kinachotakiwa,” alisema.
Pamoja na hayo, aliishukuru
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuendelea kushirikiana na jumuiya hiyo na
kuwapa kipaumbele kila wanapohitaji kuonana na uongozi wa juu wa serikali
pamoja na asasi za kiraia kwani imekuwa ikiwaunga mkono likiwemo shirika la Help
Age Internation Tanzania (HAITAN).
Comments
Post a Comment