Dk. Mwinyi ahimiza uzalishaji, ulaji mbogamboga, matunda


RAIS wa Zanzibar na Mweyekti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuna haja ya kuongeza uzalishaji wa mazao ya mboga mboga na matunda ili kukidhi mahitaji ya soko la mazao hayo nchini.

Ameeleza hayo jana wakati akizindua kituo cha taarifa na maarifa ya kilimo cha mazao hayo (Horticulture) kilichopo Mpendae Kwa Binti Hamran, wilaya ya Mjini Unguja akisema Zanzibar inahitaji tani 276,000 kwa mwaka ili kukidhi mahitaji kwa wananchi wake.

Alisema takwimu zinaonesha kuwa kila mzanzibari anahitaji kilo 146 za mazao hayo kwa mwaka na kwamba uwepo wa hoteli za kitalii, inakadiriwa wastani wa tani 2,000 zinatumika kwa mwaka katika eneo hilo.

Dk. Mwinyi akikata utepe kuashiria ufunguzi wa kituo cha maarifa ya kilimo cha hortculture

Aliongeza kuwa kiwango hicho kina thamani ya shilingi bilioni 1.6 kwa wastani wa bei za mwaka 2022 ambapo kutokana na kasi ya ukuaji wa watu ya asilimia 3.7 kwa mwaka na hivyo kufikia watu milioni 2.1 mwaka 2026 ambapo uhitaji huo utaongezeka hadi kufikia tani 319,000 mwaka 2026.

Aidha alisema Zanzibar ipo nyuma katika matumizi ya mboga na matunda hivyo anaamini wakulima wataongeza kasi ya uzalishaji wa kilimo cha mazao hayo kukidhi ukubwa wa mahitaji unaokua kila siku. 

Dk. Mwinyi akipata maelezo kuhusu kilimo cha hortculture kutoka kwa mwanaharakati wa kilimo hai, Mwatima  Abdallah Juma

Alifahamisha kuwa mwaka 2021/2022, uzalishaji wa mazao ya ‘horticulture’ Zanzibar ulifikia jumla ya tani 148,000 kiasi ambacho ni ongezeko la asilimia 68.2 katika kipindi cha mwaka 2012.

Alisema ongezeko la uzalishaji limepunguza utegemezi ambapo uagizaji wa matunda na mbogamboga kutoka nje ya nchi umepungua kutoka asilimia 80 mwaka 2014 hadi kufikia asilimia 26 mwaka 2021.

Alisema kilimo hicho pia ni muhimili wa lishe na afya bora kwa wananchi kwani utumiaji wa mazao ya mboga mboga, matunda na viungo huwapa virutubisho muhimu kwa ajili ya kujenga na kutunza miili na kutufanya wawe na afya njema.

Akizungumzia upatikanaji wa masoko alisema huchochea kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa bidhaa za aina yoyote katika nchi kwani inakadiriwa kuwa asilimia zaidi ya 90 ya mazao na bidhaa zote za ‘horticulture’ zinazozalishwa hapa Zanzibar.

Dk. Mwinyi akipata maelezo kuhusu vifaa vinavyotumika katika tasnia ya hortculture kutoka kwa mmoj ya wadau wa kilimo hicho

Alisema TAHA ni chombo muhimu katika kuendeleza uchumi wa Zanzibar na uwepo wao umekuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo ya ‘horticulture’ hapa nchini. 

Hata hivyo alisema kufunguliwa kwa kituo hicho, kunabainisha nafasi mpya ya Zanzibar katika ukanda wa Afrika ya Mashariki kama miongoni wa vinara wa uzalishaji wa mazao ya bustani na ‘horticulture’.  


Dk. Mwinyi aliitaka Wizara ya Kilimo, TAHA na wadau wengine kuimarisha jitihada katika kuongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali ya mboga mboga ili kukidhi mahitaji ya masoko ya ndani na ziada kusafirisha nje.

Akimkaribisha Rais Mwinyi Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Shamata Shaame Khamis, alisema wizara yake ni moja ya taasisi inayopata fursa kutoka kwa wadau wa maendeleo ikiwemo taasisi ya TAHA kuendeleza sekta ya kilimo nchini.

Nae Mtendaji Mkuu wa TAHA, Jacqueline Mkindi, alisema taasisi hiyo imefanikiwa kuwaunganisha wakulima zaidi ya 1,000 kwa kuwapatia mafunzo ya kilimo cha mbogamboga na matunda ambao wanaendelea na kazi hiyo katika maeneo ya Zanzibar.

Dk. Mwinyi akipokea zawadi toka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TAHA, Jacqueline Mkindi

Mkindi aliongeza kuwa kabla ya kuanzishwa kwa miradi ya kilimo biashara, Zanzibar ilikuwa inaagiza mazao ya matunda na mbogamboga kwa asilimia 80 kutoka maeneo mbali mbali.

Alieleza kuwa asilimia 42 ya wakulima wa Zanzibar wanalima kilimo cha ‘hortculture’ ambao wanaendelea na kunufaika na kilimo hicho kupitia TAHA.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango