Masheha, Madiwani wapewa elimu miradi ya TASAF

NA MWANDISHI WETU, PEMBA

VIONGOZI wa Shehia na Wadi kisiwani Pemba wametakiwa kusimamia vyema miradi ya kuwaondolea wananchi umaskini ili itoe matokeo chanya.

Ofisa Mdhamini Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango Pemba, Abdullwahab Said Bakari, alitoa wito huo na kusema kufanya hivyo ni kutekeleza malengo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) ya kupunguza umaskini kwa wananchi na kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi.

Alisema serikali imepanga mpango wa kupunguza umaskini na kuongeza ukuaji wa uchumi jumuishi unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF) ambayo imeweka sifa kwa walengwa wake.

Bakari alieleza hayo wakati akifungua mafunzo kwa Masheha na Madiwani wa mkoa wa Kusini Pemba yaliyolenga kuwajengea uwezo viongozi wanaosimamia shughuli za mpango wa kunusuru kaya maskini Tanzania, ulioandaliwa na TASAF Pemba.

“Hivi sasa kuna changamoto nyingi nyinyi kutoka kwa walengwa, Masheha na Madiwani mnatakiwa kuwa mabalozi, pia wasemaji wazuri wa kuisema TASAF kwa jamii”, alisema.

Aidha alisema changamoto kubwa zifikishwa kwa watendaji ili kupatiwa ufumbuzi, yale maneno ambao sio sahihi yataweza kupatiwa ufafanuzi, ili changamoto zinazotokezea za wananchi zinahitaji kutatuliwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Tanzania, Mkurugeni Uratibu, Haika Shayo, alisema mafunzo hayo yatasaidia kufanikisha lengo la mpango, kwani kutakuwa ni mwanzo mzuri kwa viongozi hao kufahamu kikamilifu juu ya masuala na shughuli mbali mbali za TASAF.

Aidha aliwataka walengwa kuhakikisha wanafungua akaunti benki kwa ajili ya kupokelea fedha zao, kwani suala la fedha mkononi limeshaondoka,” alisema.

Naye Ofisa ufuatiliaji TASAF Pemba, Abrahman Khamis, alisema madhumuni ya mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo viongozi wanaosimamia shughuli za mpango, kuwa na uelewa wakutosha juu ya taratibu zinazotumika kusimamia na kufuatilia shuhuli za mpango.


Aidha Mratibu wa TASAF Pemba, Mussa Said, alisema lengo ni kuongeza kipato kwa wananchi, pamoja na kuongeza ujuzi kupitia miradi wanayoianzisha kwenye shehia zao, kwani ushirikishwaji wananchi ni jambo kubwa katika kuibua miradi ya maendeleo kupitia walengwa wa mpango wa kunusuru kaya masikini.

Hata hivyo, kwa upande wa Masheha waliahidi kwenda kusimamia kikamilifu, shughuli zote za TASAF  zinazofika katika shehia zao, kwani wao ndio viongozi wa  serikali kwenye ngazi nya shehia.

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango