Wanafunzi MCC, MSJ watakiwa kusoma kwa bidii
WANAFUNZI
wanaosomea fani ya habari katika chuo cha Mwenge Community Center (MCC) na
Morogoro School of Journalis (MSJ) wametakiwa kusoma kwa bidii ili kuwa
wataalamu wazuri wa fani ya habari wanapomaliza masomo yao.
Alisema hatua hiyo
itawasaidia kuwa ujasiri katika kutekeleza vyema majukumu ya kuisemea jamii
kwaniu tasnia hiyo ni muhimu katika kuchochea maendeleo na ustawi wa jamii.
“Leo mpo chuoni lakini mtakapotoka hapa mtakwenda kuitumikia jamii hivyo kuna umuhimu kwenu kujikita katika masomo ili maarfa mnayoyapa mkayatumie kuimarisha ustawi wa jamii na maendeleo ya nchi”, alieleza Mfaume.
Sambamba na hayo
aliwataka waandishi wa habari hapa nchini kuacha mihemko wanapotekeleza
majukumu yao badala yake kuzingatia misingi na maadili ya tasnia hiyo ili kuepuka
kuleta taharuki nchini lakini pia kufanya kazi kwa ufanisi.
Nae Mkufunzi wa
chuo hicho, Omar Abdalla Juma, alipongeza uamuzi wa klabu hiyo kwenda katika
chuo hicho na kukutana na wanafunzi kuwakumbusha wajibu wao na kuwaonesha
mahali wanapoweza kufikia pindi wanapomaliza masomo yao.
“Hatua hii
imeonesha ni namna gani jumuiya hii inathamini taasisi zinazotoa taaluma ya
uandishi kama hii ambayo imetoa watendaji wengi wa vyombo vya habari na fani
nyengine zinazofundishwa hapa”, alieleza Omar.
Aidha aliwaomba
wanafunzi hao na waandishi wa habari waliopo kazini kuendelea kufanya kazi zao
kwa kuzingatia maadili na miongozo ili wazidi kutoa sifa njema ya chuo hicho na
kada ya uandishi wa Habari.
Nae Kaimu Mkuu wa chuo
cha MSJ, Mohamed Ali Mohamed, aliwahimiza wanafunzi hao kuthamini juhudi
zinazochukuliwa na wadau mbali mbali kuiimarisha kada hiyo hivyo wanapaswa
kuzingatia nidhamu na maadili wanapopata nafasi ya kwenda kuitumikia jamii.
Hata hivyo aliwashauri
kujiungana klabu hiyo ili wazidi kupata uelewa na uwezo wa kujiamini wanapokuwa
katika majukumu yao ya kazi na kuishukuru ZPC kwa msaada wa vitabu na majakreti
ya usalama walivyovitoa kwa chuo hicho.
Mapema akielezesa
madhumuni ya mkutano huo, Katibu Mkuu wa ZPC, Mwinyimvua Abdi Nzukwi, alieleza
kuwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Habari ambapo klabu hiyo
iliona ni vyema kukutana na wanafunzi wa vyuo vya Habari ili kuwajegea uwezo wa
kujieleza kama moja ya haki zinazotambulika kikatiba.
“Mhadhara huu
unalenga kuibua mijadala juu ya haki na uhuru wa kujieleza lakini pia kuangalia
nafasi za asasi za kihabari zinazvyoweza kukuza Uhuru wa Habari na taaluma ya
uandishi wa Habari nchini”, alieleza.
Wakizungumza katika
mhadhara huo, baadhi ya wanafunzi wanaosoma chuoni hapo waliishukuru ZPC kwa
kwenda kuwapatia taaluma hiyo na kuwaonesha njia ya kutekeleza majukumu yao
pale watapokuwa wamemaliza masomo yao.
Akifunga mhadhara huo, Makamu Mwenyekiti
wa Klabu hiyo, Tabia Makame Mohammed, aliwataka wanafunzi hao kuvunja ukimya
dhidi ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia vinavyofanywa na baadhi ya watendaji
wa vyombo vya Habari.
Alieleza kuwa kuna malalamiko ya wanafunzi
kufanyiwa vitendo hivyo wanapokwenda kwenye mazoezi ya vitendo katika vyombo
vya habari, jambo ambalo ni kinyume na maadili ya uandishi wa habari na
haki za binaadamu.
Mbali na mkutano
huo ZPC ilikabidhi vitabu vinavyohusiana na uandishi wa habari kwa lengo la kuimarisha maktaba ya chuo hicho
kuwasaidia wanafunzi kuongeza maarifa lakini pia makoti ya usalama kwa ajili ya
waandishi wa redio ya chuo hicho.
Comments
Post a Comment