Dk. Mwinyi aeleza dhamira CCM kufanya vikao vikuu Z'bar

NA MWANDISHI WETU

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameahidi kuwa chama hicho kitafanya mkutano mkuu wake taifa ndani ya visiwa vya Zanzibar ilimkutoa fursa kwa wajumbe kushuhudia maendeleo yaliyopatikana.


MAKAMU Mwenyekit wa CCM Zanzibar, Dk. Hussein  Ali Mwinyi, akisalimiana na mmoja ya wenyeviti wa CCM wa mikoa waliofika ikulu kumsalimia.

Dk. Mwinyi ambaye pia ni na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi aliyasema hayo Ikulu Zanzibar alipokua akizungumza na Wenyeviti wa mikoa wa chama hicho kutoka mikoa yote ya Tanzania waliofika kumsalimia.

Alisema CCM Zanzibar, itahakikisha inalifanikisha azma hiyo na kuwezesha uptikanaji wa rasilimali zote ikiwemo eneo muafaka la kuhudumia wajumbe wote wa mkutano huo na mikutano mengine ya Halmashauri Kuu taifa ikiwa ni pamoja na kujenga ukumbi mkubwa wa mikutano.

Alieleza kuwa uwepo wa ukumbi huo utaiwezesha nchi nzima kuwa Zanzibar ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya chama hicho.



Aidha Dk. Mwinyi, alimpongeza Mwenyekiti wa CCM taifa ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassa kwa kuwaalika viongozi hao wa chama kuhudhuria Tamasha la Kizimkazi lililoanza siku chache zilizopita.

Katika hatua nyengine, Dk. Mwinyi alisifu uamuzi wa viongozi hao kutembelea Zanzibar kwani ni moja ya njia ya kukuza na kudumisha ushirikiano, umoja na mshikamano ndani ya chama, hivyo aliwaomba viongozi hao kutembelea maeneo mengine na kujionea miradi ya maendeleo ya chama hicho kwa kubadilishana uzoefu.

Akizungumza Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mjini Magharibi, Talib Ali Talib, alimueleza Makamu Mwenyekiti huyo jinsi walivyoupokea ugeni huo na kuutembeza maeneo mbali mbali ya historia ya Zanzibar ikiwemo Mji Mkongwe wa Zanzibar na kuangalia maeneo mengine ya Utalii.

Naye, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi. Akizungumza kwa niaba ya Wenyeviti wenzake alimpongeza Dk. Mwinyi kwa hatua kubwa za maendeleo aliyoifanikisha ndani ya kipindi kifupi cha uongozi wake.

Aidha kupitia dk. Mwinyi, Wenyeviti hao walimshukuru Mwenyekiti wa CCM taifa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan kwa mwaliko aliowapa kuhudhuria Tamasha la Kizimkazi na kujionea mandhari halisi ya Zanzibar kwa waliokuwa hawajawahi kufika.

Aidha walisifu hatua hiyo na kuitaja kuwa ni njia ya kukuza utalii wa ndani na kudumisha ushirikiano baina ya viongozi wa chama hicho wa mikoa ya Tanzania bara na zanzibar.

 

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

Uislam unakubali uzazi wa mpango