Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya

NA MWANAISHA SHARIA, MOROGORO

WAANDISHI wa habari wametakiwa kuendelea kuibua changamoto mbali mbali zinazowakabili wanawake ili wapate fursa za maendeleo zinazojitokeza nchini.

Mkurugenzi wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya alipokua akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuhusu kuandika habari za usawa wa kijinsia yaliyofanyika hoteli ya Flomi, mjini Morogoro.

Amesema wandishi wa habari wana nguvu ya kufikisha ujumbe kwa jamii hivyo wana jukumu la kuhakikisha wanatoa elimu ya usawa wa kijinsia ili kutatua changamoto zilizopo.

"Waandishi wa habari mtakapoibua kero za wanawake na kuzisemea mtaleta mabadiliko kwa wanawake hao lakini pia jamii nzima kwani kupitia kwao ukatili na ukandamizaji wanawake na watoto wa kike utaondoka”, alieleza Simbaya.



Aidha Mkurugenzi huyo amewataka waandishi waliopatiwa mafunzo hayo kutumia vizuri elimu hiyo kwa kuandika habari na kuanda vipindi kuhusu usawa wa kijinsia ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Nae Afisa Miradi anayesimamia masuala ya jinsia UTPC, Hilda Kileo, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaongezea ujuzi wandishi wa habari kuandika habari kuhusu usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake katika nyanja za uchumi, siasa na jamii.

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo, Mkufunzi Deo Tembo, amesema endapo kutakua na usawa wa kijinsia na ushirikishwaji wa wanawake katika mambo mbali mbali kutaongeza Fursa za ukuaji wa uchumi na maendeleo.

Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo Mgongo Kaitika na Zaituni Juma wameushukuru uongozi wa UTPC kwa kutoa mafunzo waliyowapatika na kuahidi kuyafanyia kazi ili kuleta mabadiliko katika jamii.

Mafunzo hayo ya siku mbili yanayohusisha waandishi wa habari 28 wanachama wa klabu za waandishi wa habari za Tanzania bara na Zanzibar yameandaliwa na UTPC ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango mkakati wake unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la watu wa Sweden (SIDA).

Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Uislam unakubali uzazi wa mpango