Uislam unakubali uzazi wa mpango

NA MWAANDISHI MAALUM

KWA muda mrefu, suala la uzazi wa mpango limekuwa na mjadala mrefu katika jamii na vyombo vya habarijuu ya kama jee ni sawa au linapingana na maelekezo ya dini ya Kiislamu?

Maelezo yamekuwa mengi na yenye aina tafauti ya maelezo, lakini ukweli na uhakika ni kwamba dini ya Kiislamu haina pingamizi juu ya uzazi wa mpango kwa vile linasaidia mzazi na mtoto kuwa na afya bora.


Sheikh Khamis Abdulhamid

Mjumbe wa Baraza la Maulamaa Zanzibar, Sheikh Khamis Abdulhamid, amesema dini ya Kiislamu haijakataza  uzazi wa mpango ambao hauna na madhara kwa pande zote mbili.

“Wakati Quran inashushwa Masahaba waliwahi kusema Quran haikutukataza kutumia njia ya mshindo (kumwanga maji ya uzazi nje) ili kupanga uzazi“, Sheikh Khamis alisemaa.

Hata hivyo, aliongeza ni muhmu kwa wanawaume kujitahidi kufuatilia na kujipanga kupata elimu ili ndoa zao ziwe na furaha kwa kuweka utaratibu maalum wa kupata watoto.

“Ikiwa mtu atasema ukikataa kuzaa nimekuacha basi hakika hio ni talaka ila hilo sio lengo,maana unaweza kusema na mkeo akachoka akafanya yeye pekee yake mkawa mnaishi kwenye ndoa ambayo sio halali”, aliongeza.

Saida Kassim (36) mama wa watoto sita mkaazi Magomeni, Unguja ni mama wa nyumbani anayejishughulisha kupika badia asubuhi kwa ajili ya kujipatia riziki.

Muonekano wa mwili wake ni wa mtu aliyechoka na dhaifu kidogo kwa sababu ya kupitia changamoto kadhaa za uzazi.

Zaidi ya hayo sasa anapambana na changamoto za malezi. Mtoto wake wa mwisho ni wa umri wa miezi saba  na aliyemtangulia ana mwaka mmoja na miezi miwili

Tabaan watoto  hawa wawili bado hawajitambui na  wanamtegemea yeye kwa huduma zote, kama kulishwa, kunyweshwa maji, kuoshwa na kadhalik. Usafi wa nyumba na biashara yake ni mambo ya lazima kwamaisha yake na watoto wake.

Saida anatamani kupumzika kuzaa ili apate muda wa kutosha kuwatunza watoto wake na kurudisha hali yake ya mwili.

Lakini amekabiliwa na kikwazo kikubwa. Nacho ni mume wako hataki kuliskia suala la uzazi wa mpango kwa na licha ya kutotaka kulisikia.

Vile vile ana hofu iliyotokanana na maneno yaliyozagaa kwenye jamii juu ya madhara kadhaa yanayowapata wanawake wanaojiunga na uzazi wa mpango.

Mama huyu wa watoto sita anasema mwenza wake hataki wawe na uzazi wa mpango wakati hakuna kati ya watoto wake sita waliopishana miaka miwili kwenye kujifungua.

Kwa maana hio huyu mama amekuwa akibeba mimba moja baada ya nyengineuda mfupi tu baada ya kujifungua. Kwa mujibu wa tafiti nyingi na ushuhuda tunaouona katika maisha hii ni hali hatarishi kwa mzazi na watoto wake.

“Mume wangu hataki , anachotaka ni starehe na furaha  yake ni mimi kuzaa, sasa naogopa na nimechoka sana” amesema Saida kwa sauti ya unyonge huku akiwa anamnyonyesha mtoto wake mdogo na mwengine anamsubiri amhudumie.

Wakati wa mazungumzo hayo, baba mzazi alikuwa hayupo na hapakuwepo mtu mwengine karibu wa kumsaidia malezi.Ni hali ya kusikitisha.

Ni dhahiri hali ya kutokukubaliana kwa pamoja kama familia inamrudisha nyuma Saida kiafya na kiuchumi kwa familia.

Mama huyo ameshindwa kufanya maamuzi sahihi ya kulinda afya na maisha yake kwa sababu ya hofu ya kumuudhi mwenza wake, lakini zaidi kutokana na yeye na mmewe kutopata elimu juu ya faida na furha iliopo katika uzazi wa mpango.

“Kwa mfano nikipata mimba watoto wangu wanahangaika, maana mimi kila siku hospitali kuumwa, Hivyo kwao wao kusoma ni shida na wakati mwengine hakuna mtu anayewashughulikia watoto “, alieleza Bi Saida.

Ripoti ya Afya ya Zanzibar ya mwaka 2022 inaonesha inaonesha  matumizi ya uzazi wa mpango anzibar yameshuka  kutoka asilimia 7.5 (yaani watu 75 kwa kila watu 1,000a) kwa mwaka 2020 hadi  asilimia 6.9 ( yaani watu 69 kwa kila kwa kila watu 1,000) kwa mwaka 2021.

Hii inaashiria kuwepo kwa athari kubwa zaidi na hatari ya mama na mtoto kupoteza maisha.

Juma Mfaume Ali (32), Mwalimu wa sKuli ya Maandilizi binafsi iliyopo Magomeni  anakiri kutokuwepo elimu ya  afya ya uzazi kwa usahihi kwenye jamii.

Ameeleza kuwa hali hii ipo zaidi kwa wanaume na aliwataka viongozi wa dini kuzungumzia hali hii kwa upana wake na madhara yanayotokana na maamuzi  ya upande mmoja, kama ya mume kushikilia alitakalo.

“Haya mambo hayasemwi kwa upana na athari zake kwa wanawake na kwa upande wa dini kupanga uzazi kuaonekana jambo la kizungu wakati dini inatupa nafasi ya kumpumzisha uzazi mwanamke kwa miaka miwili”, alieleza Juma.


Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake, Ummulkulthum Omar, alisema taarifa za afya ya uzazi kwa wanafamilia kwa usahihi zinapatikana vituo vya afya pale mama mjamzito anapoanza kliniki kwa wakati.

“Uzazi wa mpango ni afya kwa sio familia ya mama au mtoto tu bali kwa ustawi wa jami na nchi kwa jumla’, alisema.

Mradi wa Afya ya Uzazi kwa wanawake na vijana umefadhiliwa na Shirika la Wellspring Philanthropic Fund la Marekani ambapo kwa sasa unatekelezwa na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA kwa pande zote mbili za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa lengo la kujenga uelewa wa jamii juu ya umuhimu wa kufuata njia sahihi za uzazi wa mpango.


Comments

Popular posts from this blog

ZALIRI, FLI zaingia makubaliano kuimariusha sekta mifugo

Ibueni changamoto zinazokamisha usawa wa kijinsia - Simbaya